Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 2:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Basi mumupokee kwa furaha kubwa sana kwa jina la Bwana. Munapaswa kuwapa watu wa namna hii heshima,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 2:29
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni furaha kabisa! Mujumbe anatokea kwenye mulima. Anatangaza habari njema za amani, heri, na ukombozi. Anauambia Sayuni: Mungu wako anatawala!


Na katika muji wowote watu watakapokataa kuwakaribisha, mutoke kule na mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu. Jambo hili litakuwa ushuhuda juu yao.”


Kweli, kweli ninawaambia: mutu anayemupokea yule ninayemutuma, ananipokea mimi vilevile; na mutu anayenipokea, anamupokea yule aliyenituma.”


Kila siku walikuwa wakikusanyika pamoja katika hekalu, nao walikula chakula pamoja katika nyumba zao kwa furaha na katika unyenyekevu.


Watu wakatuheshimu sana, na wakati tulipoondoka kwa njia ya chombo kwa kuendelea wakatupatia vitu vyote tulivyohitaji kwa safari yetu.


Na namna gani watahubiri ikiwa hawatumwi? Ni kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia jinsi kunavyofurahisha kuja kwa wale wanaoleta habari njema.”


Mumupokee kwa ajili ya Bwana, kama vile watu wa Mungu wanavyopaswa kufanya. Mumusaidie katika kila jambo atakalohitaji toka kwenu, maana yeye amewasaidia watu wengi na hata mimi peke yangu vilevile.


Kama Timoteo akifika, mujikaze kumupokea vizuri kati yenu kwa sababu yeye anafanya kazi ya Bwana kama mimi mwenyewe.


nao wamenifariji kama vile walivyowafariji ninyi wenyewe. Inafaa kuwakumbuka watu kama hawa.


Kwa maana, mutu anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, lakini ni yule anayesifiwa na Bwana.


Mutufungulie moyo wenu! Hatukumukosea mutu yeyote, hatukumunyanganya mutu yeyote, wala kumupotosha mutu yeyote.


Hivi ninamutuma kwenu kwa haraka kusudi mupate kufurahi wakati mutakapomwona tena na huzuni yangu ipate kupunguka.


Mufungwa mwenzangu Aristarko anawasalimia. Naye Marko, binamu wa Barnaba anawasalimia vilevile. (Mumekwisha kupata maagizo juu ya Marko; akifika kwenu mumupokee vizuri).


Wandugu, tunawaomba muwaheshimu sana wale wanaoshugulika na kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwaonya.


Wazee wa kanisa wanaoongoza kazi yao vizuri wanastahili kupokea mushahara mara mbili, hasa zaidi wale wanaojitolea kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha.


Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Kwa sababu hiyo wakati nitakapokuja, nitaonyesha wazi mambo yote anayotenda akitusingizia sisi maneno mabaya. Lakini hatosheki na mambo yale, yeye mwenyewe anakataa kukaribisha wandugu wale wanaokuwa katika safari. Na wale wanaotaka kuwakaribisha, anawakataza na kuwafukuza katika kanisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ