(Hakusema maneno haya kwa sababu aliwasikilia wamasikini huruma, lakini kwa sababu alikuwa mwizi. Ni yeye aliyekuwa akichunga mufuko wa feza, naye alikuwa akijitwalia mali toka ndani yake.)
Munajua ninyi wenyewe namna Timoteo alivyojionyesha kwamba anastahili, kwa maana alitumika kazi ya kueleza Habari Njema pamoja nami kama vile mwana anavyotumika na baba yake.
Naye Yesu anayeitwa Yusto, anawasalimia ninyi vilevile. Kati ya Wayuda walioamini ni hao watatu tu ndio wanaotumika pamoja nami kwa ajili ya kazi inayoelekea Ufalme wa Mungu, nao wamenifariji sana.
Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
Kama ukiwaelezea waziwazi wandugu maneno hayo, utakuwa mutumishi mwema wa Kristo Yesu, mwenye kukulishwa kiroho na maneno ya imani na mafundisho mazuri uliyoshika kabisa.
Ninakumbuka vilevile imani yako isiyokuwa ya udanganyifu, imani ile tate muzaa mama yako Loisi na mama yako Euniki waliyokuwa nayo. Ninajua hakika kwamba wewe vilevile uko nayo.
Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,
Saulo alipomaliza kuzungumuza na Daudi, Yonatani mwana wa Saulo alivutwa sana na Daudi, akamupenda kwa moyo wake wote kama alivyojipenda yeye mwenyewe.