Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 mukiwatangazia habari inayoleta uzima. Hivi nitapata sababu ya kujivuna Siku ile ya kurudia kwa Kristo kwa maana itakuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba bidii yangu na kazi yangu havikupotea bure.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 2:16
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninataka kutimiza mapenzi yako, ee Mungu wangu; sheria yako ninaishika kwa moyo wangu wote!”


Ee Mungu, wewe umenifundisha tangu ujana wangu; tena na tena, ninatangaza matendo yako ya ajabu.


Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.


Neno ninalowaambia katika giza, muliseme muchana kati. Vilevile neno munalosikia kwa siri, mulitangaze mukisimama juu ya paa ya nyumba.


“Nami ninawaambia: kila mutu anayenikubali mbele ya watu, Mwana wa Mutu atamukubali vilevile mbele ya wamalaika wa Mungu.


Roho ndiye anayeleta uzima; mwili hauwezi kufaa kitu. Maneno haya niliyosema nanyi, ndiyo Roho na uzima.


Simoni Petro akamujibu: “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unasema maneno ya uzima wa milele.


“Wandugu zangu, ninyi wazao wa Abrahamu na ninyi watu wa mataifa mengine munaokuwa hapa kwa kumwabudu Mungu, habari hii ya wokovu imetumwa kwetu!


Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Ni kwa sababu hiyo ninakimbia nikiwa na shabaha ya kushinda. Mimi ni kama mupiganaji wa ngumi asiyepiga katika hewa.


maana munayafahamu sasa kwa sehemu tu. Kwa Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu mutaweza kujivuna kwa ajili yetu kama vile tutakavyojivuna kwa ajili yenu.


Nilienda kule kufuatana na agizo nililopata katika maono. Halafu nikakusanyika na waongozi kwa upekee. Nikawaelezea Habari Njema ninayohubiri kati ya mataifa mbalimbali kusudi kazi yangu ya mbele au ya sasa isipotee bure.


Ninawaogopea, kwa maana inawezekana kwamba nimesumbuka bure kwa ajili yenu!


kusudi mupate kutambua mambo yanayokuwa bora zaidi. Kwa hivi mutakuwa safi pasipo kosa kwa Siku ile ya kurudia kwa Kristo.


Ninajua hakika kwamba Mungu aliyeanza kazi hii njema ndani yenu, ataitimiza mpaka siku ile ya kurudi kwa Yesu Kristo.


Ninyi peke yenu tu ndio tumaini, furaha, na taji ya ushindi tutakavyojivunia wakati Bwana Yesu Kristo atakaporudia.


Ni kwa sababu hiyo, nilipoona kwamba siwezi kuendelea kungojea, nilimutuma Timoteo kusudi nipate kujua habari ya imani yenu. Niliogopa kwamba labda yule mushawishi Shetani amejaribu kuwaangusha ninyi na kwamba kazi yote tuliyofanya kwenu imepotea bure.


Kwa maana Neno la Mungu ni lenye uzima, na lina nguvu; ni kali kupita upanga unaokata ngambo mbili. Linapenya hata linatenga moyo na roho na hata viungo na ubongo. Nalo linatambua nia na mawazo ya mutu.


Kwa maana mumezaliwa upya, kwa nguvu za neno la Mungu lenye uzima na linalodumu hata milele. Nanyi si kama watoto waliozaliwa na wazazi wenye mwili huu unaokuwa wa kufa, lakini watoto waliozaliwa kwa nguvu ya uzazi usioweza kufa.


Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ