Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 2:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 2:15
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Humo kulikuwa viti vya kifalme kwa kuamua maneno, ndivyo viti vya ukoo wa Daudi.


nao Waisraeli waliona uso wake unangaa. Halafu Musa alifunika tena uso wake kwa kitambaa mpaka alipokwenda kuongea na Yawe.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Kinywa changu kitasema maneno ya haki, hakuna udanganyifu wala upotevu katika midomo yangu.


Simama, ee Sayuni uangaze; maana mwangaza unatokea kwa ajili yako, utukufu wa Yawe unakuangazia.


Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.


Basi mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni anavyokuwa mukamilifu.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Lakini muwapende waadui zenu, muwatendee mema na muwakopeshe pasipo kutumainia kurudishiwa kitu. Halafu mutapewa zawadi kubwa na mutakuwa kweli watoto wa Mungu Mukubwa kwa sababu yeye ni mwema kwa watu waovu wasiokuwa na shukrani.


Yoane alikuwa kama taa inayowaka na kuangaza, na ninyi mulipendezwa kufurahishwa na mwangaza wake kwa muda.


Petro akazidi kusema maneno mengine ya kuwaonya na kuwatia moyo, akisema: “Mujiokoe toka kati ya kizazi hiki kipotovu!”


Na hata kati yenu kutatokea watu watakaotoa mafundisho ya kupotosha wengine kusudi wawavute waamini kuwafuata.


Watu wote wanajua namna munavyomutii Bwana, na kwa sababu hii ninafurahi kwa ajili yenu. Lakini ninataka mukuwe wenye hekima kwa kutenda mema, na mukuwe safi mukijitenga na mambo mabaya.


Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.


Alitaka hivi kujipatia yeye mwenyewe kanisa tukufu na takatifu, lisilokuwa na taka wala kikunjo wala kilema chochote.


Lakini ninyi mumekosa uaminifu kwake, ninyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu, ninyi ni kizazi kiovu na kipotovu.


kusudi mupate kutambua mambo yanayokuwa bora zaidi. Kwa hivi mutakuwa safi pasipo kosa kwa Siku ile ya kurudia kwa Kristo.


nilikuwa na bidii sana hata nilitesa kanisa. Kuelekea mambo ya kuhesabiwa kwa njia ya kushika Sheria, mimi sikupatikana na kosa lo lote.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Inafaa wapimwe kwanza, na kisha kama hawakuonekana na kosa, wataweza kutumika kama wasaidizi wa kanisa.


Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.


Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.


Wale wenye kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watu kusudi wengine wapate kuogopa vilevile.


Hayo ndiyo maneno unayopaswa kuwaagiza wajane kusudi wasikuwe na mashitaki.


muzee wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja nao watoto wake wanapaswa kuwa waamini na wasioshitakiwa neno juu ya mwenendo mubaya au juu ya kukosa utii.


na kuiba vitu vyao. Lakini wajionyeshe kila mara kuwa waaminifu kamili, kusudi wapate kuheshimisha mafundisho juu ya Mungu Mwokozi wetu katika mambo yote.


Haya ndiyo maneno unayopaswa kufundisha, ukiwaonya watu na kuwakaripia kwa mamlaka yote. Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Kwa sababu hiyo, wapendwa wangu, mukiwa munangojea mambo yale, mufanye bidii apate kuwakuta safi bila kosa lolote na mukae na amani pamoja naye.


Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ