Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 2:14
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walinungunika ndani ya hema zao, wala hawakumusikiliza Yawe.


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Kundi hili la watu waovu litaendelea kuninungunikia mpaka wakati gani? Nimechoka na haya manunguniko ya Waisraeli juu yangu!


Watu wale walipopokea mushahara ule, wakamunungunikia mwenye shamba.


Marasi hii ingeweza kuuzishwa kwa bei ya vikoroti mia tatu vya feza na kugawanyia wamasikini mali ile.” Na wakamukasirikia yule mwanamuke vikali.


Waliporudi kwenye wanafunzi wengine, wakaona kundi la watu wengi wakiwazunguka na walimu wa Sheria wakibishana nao.


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Basi Paulo na Barnaba wakapingana na kubishana nao vikali sana juu ya jambo hili. Na kwa hiyo wandugu waamini wakaagiza Paulo na Barnaba pamoja na watu wengine kati yao waende Yerusalema kusemezana na mitume na wazee wa kanisa la kule juu ya maneno yale.


Kwa hiyo Paulo na Barnaba wakabishana vikali hata wakatengana. Barnaba akaondoka pamoja na Marko, wakaingia ndani ya chombo na kwenda katika kisanga cha Kipuro.


Mabishano yalipoendelea, Petro akasimama na kusema: “Wandugu zangu, munajua kwamba Mungu alinichagua pale zamani kati yenu kusudi nihubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine wapate kuisikia na kuamini.


Katika siku zile, kufuatana na jinsi hesabu ya wanafunzi wa Yesu ilivyokuwa ikizidi kuongezeka, kulitokea manunguniko kati ya Wayuda waliosema Kigriki na Wayuda waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigriki walinungunika kwa sababu wajane wao walisahauliwa wakati wa kugawanya vifaa vya kila siku.


Kama ikiwezekana, kwa upande wenu, muishi katika amani na watu wote.


Mumupokee yule anayekuwa zaifu katika imani pasipo kubishana naye juu ya mawazo yake.


Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.


Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.


Lakini kama mukiumana na kukulana kama nyama wa pori, muangalie vizuri musiteketezane.


Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.


Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.


Muwape heshima kubwa na kuwapenda kwa ajili ya kazi yao. Mukuwe na amani kati yenu.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.


Lakini mukiwa na wivu wenye kuchangana na uchungu katika mioyo yenu pamoja na roho ya ugomvi, musijivune wala musigeuze maneno ya kweli kuwa uongo.


Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!


Aepuke mabaya, atende mema, atafute amani na kuifuatilia.


Mukaribishane ninyi kwa ninyi pasipo kunungunika.


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ