Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”
Basi Paulo na Barnaba wakapingana na kubishana nao vikali sana juu ya jambo hili. Na kwa hiyo wandugu waamini wakaagiza Paulo na Barnaba pamoja na watu wengine kati yao waende Yerusalema kusemezana na mitume na wazee wa kanisa la kule juu ya maneno yale.
Kwa hiyo Paulo na Barnaba wakabishana vikali hata wakatengana. Barnaba akaondoka pamoja na Marko, wakaingia ndani ya chombo na kwenda katika kisanga cha Kipuro.
Mabishano yalipoendelea, Petro akasimama na kusema: “Wandugu zangu, munajua kwamba Mungu alinichagua pale zamani kati yenu kusudi nihubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine wapate kuisikia na kuamini.
Katika siku zile, kufuatana na jinsi hesabu ya wanafunzi wa Yesu ilivyokuwa ikizidi kuongezeka, kulitokea manunguniko kati ya Wayuda waliosema Kigriki na Wayuda waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigriki walinungunika kwa sababu wajane wao walisahauliwa wakati wa kugawanya vifaa vya kila siku.
Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.
Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.
Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.
Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.