Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 na kila mutu akubali kwamba Yesu ni Bwana, naye Mungu Baba atatukuzwa kwa njia hiyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 2:11
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


Ameniokoa kutoka waadui zangu, Ee Yawe, ulinitukuza juu ya wapinzani wangu na kuniponyesha kutoka watesaji wakali.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


“Kila mutu anayenikubali mbele ya watu, nami nitamukubali vilevile mbele ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.


Hata hivi wengi kati ya wakubwa wa Wayuda wakamwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Wafarisayo, hawakushuhudia kwamba wameamini. Waliogopa kwamba watatengwa wasiingie katika nyumba ya kuabudia.


Munaniita ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ na munasema kweli, maana ni vile ninavyokuwa.


Basi kama mimi ninayekuwa Bwana na Mwalimu wenu nimewanawisha miguu, ninyi vilevile munapaswa kunawishana miguu.


Nami nitafanya chochote mutakachoomba kwa jina langu, kusudi Baba atukuzwe kwa njia ya Mwana.


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile.


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


“Kwa hiyo watu wa taifa la Israeli wajue hakika kwamba yule Yesu muliyemutundika juu ya musalaba, Mungu amemufanya kuwa Bwana na Masiya!”


Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Bwana anasema: Kama vile ninavyoishi, kila mutu atapiga magoti mbele yangu, na kila mutu ataitikia kwamba mimi ni Mungu.”


Ni kwa sababu hii Kristo alikufa na kufufuka kusudi apate kuwa Bwana wa waliokufa na wa wanaokuwa wazima vilevile.


Vilevile ilikuwa kusudi watu wa mataifa mengine wamutukuze Mungu kwa huruma yake, kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa, nitakuimbia sifa.”


Kwa sababu hii ninataka mufahamu kwamba hakuna mutu ambaye anaongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema: “Yesu alaaniwe,” na hakuna mutu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana,” kama asipoongozwa na Roho Mutakatifu.


Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, yeye ni wa dunia, lakini Adamu wa pili alitoka mbinguni.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Kila mutu anayesema kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaungana naye, na mutu yule anaungana na Mungu.


Mutatambua Roho wa Mungu kwa njia hii: kila mutu anayesadiki kwamba Yesu Kristo amekuja katika hali ya kimutu yuko na Roho wa Mungu.


Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika dunia. Watu hawa hawakubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili wa kimutu. Yule asiyekubali vile ni mudanganyifu na mupinga Kristo.


Yule atakayeshinda atavalishwa nguo nyeupe, nami sitafuta jina lake kati ya majina yanayoandikwa katika kitabu cha uzima. Nami nitamutetea mbele ya Baba yangu na mbele ya wamalaika zake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ