Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 1:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Basi niko na uhakika juu ya jambo hili nami ninajua kwamba nitabaki. Nitakaa pamoja nanyi kwa kuwasaidia kusudi mupate kuendelea na kuwa na furaha katika imani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 1:25
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uwaarifu kwa vitambulisho wale wanaokuheshimu, wapate kuuepuka mushale.


Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


“Nilikuwa nikizungukazunguka kati yenu ninyi wote nikitangaza Ufalme wa Mungu. Lakini sasa, ninajua kwamba hakuna hata mumoja atakayeniona tena.


Basi, Mungu anayekuwa musingi wa matumaini, awajaze furaha kamili na amani kutokana na imani yenu; hata tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mutakatifu.


Kwa maana sitasubutu kuongeza kitu kingine, isipokuwa tu kile Kristo alichotimiza kwa njia yangu kusudi watu wa mataifa wapate kumutii Mungu. Alifanya vile kwa njia ya yale aliyoniwezesha kusema na kutenda,


Nami ninajua kwamba wakati nitakapokuja kwenu, nitakuja na baraka nyingi sana kutoka kwa Kristo.


Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.


Hatutafuti kuwaamuru ninyi juu ya mambo yale munayopaswa kuamini, maana munasimama imara katika imani. Lakini tunataka kutumika pamoja nanyi kusudi mupate kufurahi.


Lakini jambo la lazima zaidi kwa ajili yenu, mimi niendelee kuishi.


Nami ninamutumainia Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja kuwaona bado kidogo.


Lakini pamoja na maneno haya, unitayarishie vilevile pahali pa kukaa, maana ninatumaini kwamba Mungu atajibu maombi yenu, na kunijalia nipate kurudishwa tena kwenu.


Ninyi munamupenda ijapokuwa hamujamwona, na munamwamini ijapokuwa sasa hamumwoni. Na zaidi ya ile munashangilia kwa furaha isiyoweza kuelezwa, inayojaa utukufu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ