Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.
Kwa maana, tunajua kwamba hema hii tunayoishi ndani yake hapa katika dunia, maana yake mwili wetu, itakapobomolewa, Mungu atatupatia makao mengine mbinguni. Nayo ni nyumba aliyoijenga yeye mwenyewe na inayodumu milele.
Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.
Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.
Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.
Tena nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikisema: “Andika maneno haya: ‘Heri tangu sasa kwa watu wanaokufa wakimwamini Bwana!’ ” Naye Roho anasema: “Ndiyo, ni kweli. Watapumzika toka katika masumbuko yao, kwa maana matendo yao yatafuatana nao.”