Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 1:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 1:20
41 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uniimarishe sawa ulivyoahidi, nami nitaishi; usikubali nifezeheke katika tumaini langu.


Moyo wangu ukuwe mukamilifu juu ya masharti yako, kusudi nisifezeheke.


Ninakutumainia wewe, ee Mungu wangu, usiniache nifezeheke; waadui zangu wasifurahie kushindwa kwangu.


Mumepanga kuniangusha toka nafasi yangu ya heshima; furaha yenu ni kusema uongo. Kwa maneno, munabariki, lakini ndani ya moyo munalaani.


Tumaini la mwenye haki linaleta furaha, lakini tazamio la mwovu linapotea bure.


Hakika siku nzuri zitafika na tumaini lako halitakuwa la bure.


Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe, litapata wokovu wa milele. Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.


Bwana wetu Yawe ananisaidia kwa hiyo siwezi kufazaika. Uso wangu nimeukaza kama jiwe; ninajua kwamba sitapata haya.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


(Yesu alisema maneno haya kwa kuonyesha kifo gani Petro atakachokufa na kumutukuza Mungu.) Kisha kusema maneno haya, Yesu akamwambia: “Unifuate!”


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Lakini Paulo akajibu: “Kwa sababu gani munalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari, si kwa kufungwa tu kule Yerusalema, lakini hata kufa vilevile kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”


Walipokwisha kuomba, nafasi ile walipokuwa wakikusanyika ikatikisika. Nao wote wakajazwa na Roho Mutakatifu na kuanza kutangaza Neno la Mungu kwa uhodari.


Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.


Nalo tumaini hili si la udanganyifu, kwa sababu Mungu amemimia upendo wake ndani ya mioyo yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.


Musitoe tena viungo vya mwili wenu kufanya zambi, mukivitumikisha kama vyombo vya kufanya mabaya. Lakini mujitoe wenyewe kwa kumutumikia Mungu kama watu waliofufuliwa na mutumikishe viungo vya mwili wenu kama vyombo vya kufanya haki.


(Ninatumia luga ya kawaida ya wanadamu kwa sababu ya uzaifu wenu wa kimutu). Zamani mulijitoa kabisa kuwa watumwa wa kufanya mambo machafu na maovu kwa kuishi katika machafuko. Hivi vilevile mujitoe kabisa kuwa watumwa wa kufanya haki kusudi muweze kuishi katika utakatifu.


Viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana wakati Mungu atakapowaonyesha watoto wake waziwazi.


kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia, ninaweka jiwe la kukwalisha katika Sayuni nalo ni la kuangusha. Lakini yule anayemwamini hatapata haya.”


Wandugu zangu, kila siku ninapatwa na hatari ya kufa. Na hii ni hakika sawa vile ninavyojivuna kwa ajili yenu katika kuungana kwangu na Yesu Kristo Bwana wetu.


Kwa sababu mulinunuliwa na Mungu kwa bei kali. Basi mutumie miili yenu na roho zenu kwa utukufu wa Mungu.


Yeye anashugulikia mambo mawili. Vilevile mwanamuke asiyeolewa au binti anashugulikia mambo ya Bwana. Anajitolea kwa Bwana katika mawazo na matendo yake yote. Lakini mwanamuke anayeolewa, anashugulikia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kumupendeza mume wake.


Kwa maana sioni haya hata kama nimejivuna zaidi kwa ajili ya uwezo Bwana aliotupatia sisi. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.


Na kwa sababu tunakuwa na tumaini lile, sisi tunasema kwa uhodari.


Kila wakati tunabeba mateso ya kufa kwa Yesu katika mwili wetu, kusudi uzima wa Yesu uonekane vilevile ndani ya mwili wetu.


Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, kusudi wale wanaoishi, wasiishi kwa ajili yao wenyewe, lakini kwa ajili ya yule aliyekufa na kufufuka kwa ajili yao.


Mimi nimejivuna kidogo mbele yake kwa ajili yenu, nami sikupata haya. Lakini kama vile tulikuwa tunawaambia kila mara ukweli, vilevile kule kujisifu kwetu kwa ajili yenu mbele ya Tito, kumeonekana kuwa kwa kweli.


Mimi ninawaaminia sana na kujivuna kwa ajili yenu. Katika mateso yetu yote, ninafarijiwa sana na kujazwa na furaha.


Kwa ajili ya kufungwa kwangu, wandugu wengi wamemwamini Bwana na kuwa na bidii sana ya kutangaza Neno la Mungu pasipo woga.


Hata nikitoa maisha yangu kuwa sadaka pamoja na imani yenu inayokuwa sadaka mbele ya Mungu, mimi ninafurahi na kushiriki pamoja nanyi wote.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Lakini mutu akiteswa kwa sababu yeye ni mukristo, asione haya, lakini atukuze Mungu kwa kuwa anaitwa kwa jina lile.


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ