Wanafanya matendo yao yote tu kusudi wajionyeshe mbele ya watu. Wanajifungia kwa paji za nyuso vibweta vipana vyenye vikaratasi vya Maandiko Matakatifu. Nao wanavaa kanzu zenye pembe ndefu.
Lakini kulitokea wanafunzi wengine, waliokuwa watu wa Kipuro na wa inchi ya Kurene, waliofika Antiokia. Nao wakaanza kusemezana na Wagriki vilevile, wakiwahubiri Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.
Ninaweza vilevile kugawanya mali yangu yote kwa kulisha wamasikini na hata kutoa mwili wangu uunguzwe, lakini kama sina upendo, hakuna faida ninayopata.
Kwa maana Yesu Kristo, Mwana wa Mungu ambaye Silvano, Timoteo na mimi mwenyewe tuliyemuhubiri kwenu hakukuja kusema “Ndiyo” na “Hapana.” Lakini yeye ni “Ndiyo” inayotoka kwa Mungu.
Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.
ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.
Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.
Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.