Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Wafilipi 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kutokana na hayo, walinzi wote wa nyumba ya mufalme pamoja na wengine wote, wanajua kwamba niko katika kifungo kwa sababu ninamutumikia Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Wafilipi 1:13
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”


Nao walipokwisha kuondoka wakasemezana: “Mutu huyu hakutenda neno linalomupasa kuuawa wala kufungwa.”


Kulipopita siku tatu, Paulo aliwaita wakubwa wa Wayuda waliokaa kule. Na walipokwisha kukusanyika akawaambia: “Wandugu, mimi nilifungwa kule Yerusalema na kutolewa kwa Waroma ijapokuwa sikufanya kosa lolote juu ya taifa letu wala kuvunja desturi za babu zetu.


Basi ni kwa sababu hii nimewaita kusudi tuonane na niseme nanyi, kwa maana ninafungwa na munyororo huu kwa ajili ya tumaini ambalo Waisraeli wanakuwa nalo.”


Paulo akakaa miaka miwili katika nyumba aliyokuwa akijilipia yeye mwenyewe. Alikaribisha watu wote waliokuja kumwona.


Kufuatana na mambo hayo, mimi Paulo, mufungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi watu wa mataifa mengine, ninamwomba Mungu.


Kwa hivi basi, mimi ninayekuwa mufungwa kwa sababu ninamutumikia Bwana, ninawasihi muishi sawa inavyostahili kufuatana na mwito Mungu aliowatolea.


Mimi ni mujumbe wa Habari ile Njema, ijapokuwa sasa ninakuwa katika kifungo. Basi muniombee kusudi nipate kusema kwa uhodari, sawa inavyonipasa kusema.


Sasa munashiriki pamoja nami katika vita. Ninyi muliniona nikipigana vita ile na hata sasa munasikia kama ninapigana vita ile.


Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.


Watu wote wa Mungu, na hasa zaidi wale wanaokuwa katika nyumba ya Mufalme, wanawasalimia vilevile.


Mimi ninateswa na kufungwa sawa mutenda maovu kwa sababu ninahubiri Habari Njema hii. Lakini Neno la Mungu halifungwi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ