Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Musitumike tu wakati wanapowaangalia, mukitafuta kuwapendeza. Lakini mutimize mapenzi ya Mungu kwa moyo wote mukijihesabu kama watumwa wa Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 6:6
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.


Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mudanganyifu wa Israeli hakunirudilia kwa moyo wote, lakini kwa unafiki tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa katika mbingu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Kwa sababu mutu yeyote anayefanya mapenzi ya Mungu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


Lakini asante kwa Mungu, kwa maana ninyi muliokuwa zamani watumwa wa zambi mumetii sasa kwa moyo wenu wote kanuni za mafundisho muliyopewa.


Kwa maana mutumwa aliyeitwa kuwa wa Bwana, amepewa uhuru na Bwana. Hivi vilevile mutu mwenye uhuru aliyeitwa na Kristo, ni mutumwa wa Kristo.


Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.


Kwa hiyo musikuwe wajinga, lakini mutambue mapenzi ya Bwana.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Kwa sababu hii hatuchoki kuwaombea ninyi, tangu siku tuliposikia habari zenu. Tunamwomba Mungu awawezeshe kujua kabisa mapenzi yake na kuwajaza hekima na akili inayotoka kwa Roho wake.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Lakini siku zote tunasema vile Mungu anavyotaka, kwa maana yeye aliamua kwamba tunastahili, akatupatia kazi ya kuhubiri Habari Njema yake. Sisi hatutafuti kuwapendeza watu, lakini tunataka kupendeza Mungu, anayejua siri za mioyo yetu.


Kitu Mungu anachotaka ni kwamba mukuwe watakatifu na muepuke mambo ya uasherati.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Na hayo ndiyo mapenzi ya Mungu, anayetaka munyamazishe usemi wa ujinga wa wapumbafu kwa njia ya kutenda mema.


Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.


Dunia inapita pamoja na tamaa zake, lakini mutu yule anayefanya mapenzi ya Mungu anaishi milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ