Musijenge nyumba, musilime mashamba, wala musikuwe na shamba la mizabibu. Lakini mutaishi katika mahema siku zote za maisha yenu, kusudi mupate kuishi siku nyingi katika inchi munamoishi kama wageni.
Ikuwe ni jambo la kupendeza au hapana, sisi tutaitii sauti ya Yawe, Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake kusudi mambo yatuendekee vizuri tutakapomutii Yawe, Mungu wetu.
Mufanye angalisho kutii maneno haya niliyowaamuru, kusudi mupate kufanikiwa ninyi pamoja na wazao wenu nyuma yenu milele, maana mutakuwa munatenda mazuri na kwa usawa mbele ya Yawe, Mungu wenu.
Kwa hiyo mushike masharti yake na amri zake ambazo ninawapa leo kusudi mufanikiwe, ninyi pamoja na wazao wenu, na kuishi siku nyingi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe yenu milele.”
“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.
Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.
Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.