Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ninyi watoto muwatii wazazi wenu mbele ya Bwana, kwa maana vile ndivyo inavyostahili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 6:1
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akatambua vilevile kwamba Yakobo alimutii mama yake na baba yake, akakwenda Padani-Aramu.


Basi, Israeli akamwambia Yosefu: “Unajua wandugu zako wanachunga nyama kule Sekemu. Kwa hiyo ninataka kukutuma kwao.” Yosefu akajibu: “Niko tayari.”


Hapo Yosefu akawaondoa wana wake kwenye magoti ya baba yake, kisha akainama kwa heshima.


Wana wa Yakobo walimufanyia baba yao kama vile alivyowaagiza:


Kule kwa mulima Sinai ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao. Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli, masharti mazuri na amri.


Esteri alikuwa bado hajatambulisha ukoo wala kabila lake kama vile Mordekayi alivyokuwa amemwonya asifanye. Naye Esteri akamutii kama alivyokuwa akimutii wakati wa utoto wake, alipolelewa naye.


Atashangilia mbele ya watu na kusema: “Nilitenda zambi na kupotosha usawa, nami sikuazibiwa kutokana na hayo.


Kwa hiyo, ninafuata kanuni zako zote; ninachukia kila njia ya upotovu.


Ninajua kwamba maamuzi yako ni ya haki, ee Yawe, na kwamba umeniazibu maana wewe ni mwaminifu.


Sheria ya Yawe ni kamilifu; inamupa mutu uzima mupya. Maagizo ya Yawe ni ya kuaminiwa; yanawapa wajinga hekima.


Mwana wangu, sikiliza mafundisho ya baba yako, wala usizarau mashauri ya mama yako;


Umusikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimuzarau mama yako akizeeka.


Kuna watu ambao wanalaani baba zao, wala hawana shukrani kwa mama zao.


Kama mutu akimuchekelea baba yake na kuzarau utii kwa mama yake, macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori na kuliwa na tai.


Mwana wangu, shika amri za baba yako, wala usisahau mashauri ya mama yako;


Ile amri ambayo Yonadabu mwana wa Rekabu aliwapa wana wake kwamba wasikunywe divai, imefuatwa; nao hawakunywi divai mpaka siku hii ya leo, maana wametii amri ya babu yao. Lakini mimi nilisema nanyi tena na tena, nanyi hamukunisikiliza.


Lakini Yeremia aliwaambia Warekabu hivi: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninyi Warekabu mumetii amri ya babu yenu, mukashika kanuni zake zote na kutenda kama alivyowaamuru.


Sisi tumeitii amri hiyo ya babu yetu Yonadabu mwana wa Rekabu siku zote, juu ya jambo alilotuamuru. Sisi hatukunywi divai hata kidogo; sisi wenyewe hatukunywi, wala wake zetu, wala watoto wetu wanaume au wanawake.


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Basi Yesu akarudia Nazareti pamoja nao, akaendelea kuwatii. Na mama yake alichunga maneno haya yote katika moyo wake.


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Mumupokee kwa ajili ya Bwana, kama vile watu wa Mungu wanavyopaswa kufanya. Mumusaidie katika kila jambo atakalohitaji toka kwenu, maana yeye amewasaidia watu wengi na hata mimi peke yangu vilevile.


Basi Sheria yenyewe ni takatifu na amri ni takatifu, ya haki na nzuri.


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


“Kama mutu ana mutoto mwenye kiburi na mwasi, asiyemutii baba yake au mama yake ingawa wanamwazibu,


Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.


Kwa ajili ya utukufu wa Bwana, mutii mamlaka yote ya watu: ikiwa ni mufalme anayekuwa na uwezo juu ya vyote,


Ruta akajibu: “Nitafanya yote uliyoniambia.”


Kesho yake, Daudi aliamuka asubui mapema, na akamwachia muchungaji mumoja kondoo. Alibeba chakula na kwenda kama vile alivyoagizwa na baba yake Yese. Alipofika kwenye kambi ya Waisraeli, aliwakuta wanajipanga kwenye sehemu yao ya vita na wanapiga kelele za vita.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ