Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.
Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.
Utawaambia wafungwa: Mutoke humo katika kifungo na wale wanaokuwa katika giza: Mukuje inje kwenye mwangaza! Kila pahali watakapokwenda watapata chakula hata kwenye vilima vitupu watapata malisho.
Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.
Wewe, ee Mungu, umeongoza taifa, umezidisha furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako wana furaha kama kwa wakati wa mavuno, kama vile wanaogawanya vitu walivyonyanganya wanavyofurahi.
Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.
Basi bwana wa yule mulinzi akamusifu kwa sababu alitenda kwa werevu. Kwa maana watu wa dunia hii wanatengeneza maneno yao na wenzao kwa werevu sana kuliko watu wanaopenda kuishi katika mwangaza.”
Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.
Basi muaminie mwangaza ule wakati mungali nao, kusudi mukuwe watu wa mwangaza.” Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akajiendea na kujificha mbali na lile kundi.
kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’
Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.
Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.
Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.
Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.
na wenye mafikiri yaliyotiwa katika giza. Watu hawa hawashiriki katika uzima ule unaoletwa na Mungu, kwa sababu wao ni wapumbafu na wenye mioyo migumu.
Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.
Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.
Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.
Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.