Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.
Nanyi munasema vilevile: “Chakula kiliumbwa kwa ajili ya tumbo nayo tumbo kwa ajili ya chakula.” Ndiyo, lakini Mungu ataharibu vyote viwili. Lakini mwili haukuumbwa kwa ajili ya uasherati. Mwili uliumbwa kwa ajili ya Bwana nao ni wake.
Yeye ni kichwa cha kanisa linalokuwa mwili wake. Naye ndiye asili ya uzima wa mwili ule. Yeye ndiye mwanzo, muzaliwa wa kwanza, na ndiye aliyefufuka wa kwanza, kusudi akuwe wa kwanza juu ya vyote.
Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.