Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 5:2
54 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Kisha utamuteketeza kondoo muzima juu ya mazabahu kwa kunitolea sadaka ya kuteketezwa. Harufu ya sadaka inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Yawe.


Kisha utavitwaa tena kutoka mikono yao na kuviteketeza juu ya mazabahu pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa, vikuwe harufu nzuri itakayonipendeza mimi Yawe. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto.


Lakini matumbotumbo na miguu yake atavisafisha kwa maji. Kuhani ataiteketeza yote juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Atamushika mabawa na kumupasua, lakini asimwachanishe vipande viwili. Kisha, kuhani atamuteketeza kwenye mazabahu, juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Lakini matumbotumbo na miguu ya nyama yule vitasafishwa kwa maji. Kuhani atateketeza sadaka yote juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kuhani ataviteketeza juu ya mazabahu kama chakula kinachotolewa kwa Yawe kwa moto kutoa harufu ya kumupendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Yawe.


Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini.


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


kuwa mutumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa mengine. Ninafanya kazi ya ukuhani ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu, kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuwa kama sadaka inayokubaliwa na Mungu na iliyotakaswa na Roho Mutakatifu.


Alitolewa kufa sababu ya makosa yetu na kufufuliwa kusudi tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda.


Basi mujitakase, mukiondoa ile chachu ya zamani ya zambi. Hivi mutakuwa kama donge jipya, lisilotiwa chachu, sawa vile munavyokuwa kwa kweli. Mufanye vile kwa maana Kristo amekwisha kutolewa sadaka kwa ajili yetu kama vile kondoo wa Pasaka.


Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.


Kwa maana sisi ni kama harufu nzuri iliyotolewa na Kristo kwa Mungu; na kunukia wale wanaookolewa na wale wanaopotea.


Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.


Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.


Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.


Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa.


Lakini tukitangaza ukweli kwa upendo, tutakomaa katika mambo yote na kufikia kuwa kama Kristo, ambaye ni kichwa.


Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.


Muangalie vizuri mwenendo wenu. Musiishi kama wajinga lakini muishi kama wenye hekima.


Nanyi waume muwapende wake wenu sawa vile Kristo alivyopenda kanisa na kutoa uzima wake kwa ajili yake.


Mutamujengea Yawe, Mungu wenu, mazabahu kwa mawe yasiyochongwa. Juu ya mazabahu hiyo mutamutolea Yawe, Mungu wenu, sadaka za kuteketezwa.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


Zaidi ya mambo haya yote, mukuwe na upendo, maana upendo unaunganisha kila kitu katika umoja unaokuwa mukamilifu.


Na kuelekea upendo wa wandugu waamini, si lazima kwenu kuwaandikia neno lolote, kwa maana Mungu yeye mwenyewe amewafundisha ninyi kupendana.


aliyejitoa mwenyewe kusudi awakomboe watu wote. Na huo ni ushuhuda kwa wakati uliopangwa, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wake.


Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Kila Kuhani Mukubwa anawekwa kusudi afanye kazi ya kutoa sadaka na matoleo. Kufuatana na hiyo, ilimupasa Kuhani wetu Mukubwa Kristo akuwe na kitu cha kutoa vilevile.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Basi ilikuwa lazima vitu vile vinavyoonyesha mufano wa mambo yanayopitika katika mbingu vitakaswe kwa njia ile. Lakini mambo kamili ya mbinguni yanahitaji kutakaswa kwa sadaka inayokuwa bora zaidi.


Ingekuwa hivi, ingemupasa ateswe mara nyingi tangu kuumbwa kwa dunia. Lakini sasa, wakati ukikaribia kwa mwisho, yeye alitokea mara moja tu kusudi awasamehe watu zambi kwa njia ya kujitoa mwenyewe sadaka.


Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.


Sisi tumetambua upendo kwa njia hii: Yesu Kristo alitoa uzima wake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kutoa uzima wetu kwa ajili ya wandugu zetu.


Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ