Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 5:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 5:11
48 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, akamwambia Sara: “Mimi nimemupa ndugu yako vikoroti elfu moja vya feza kwa kuwaonyesha wote wanaokuwa pamoja nawe kwamba hauna kosa. Umehakikishwa kwamba hauna kosa.”


Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.


Mwana wangu, usikubali kushawishiwa na wenye zambi.


Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu, mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.


Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.


Mwenye mazarau hapendi kuonywa, hatafuti hata kidogo maoni ya wenye hekima.


Umwazibu mwenye kuzarau naye mujinga atapata akili; umwonye mwenye akili naye atapata maarifa.


Onyo la mwenye hekima kwa mutu musikilivu ni bora kuliko pete au ushanga wa zahabu safi.


Watu wanaovunja sheria wanasifu waovu, lakini wanaoshika sheria wanapingana nao.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Watatoweka wale wanaopotosha maneno ya mutu katika tribinali, watu wanaowatega waamuzi na wanaosema uongo kwa kuwanyima haki yao wasiokuwa na kosa.


Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha, wala sikufurahi pamoja nao. Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako; kwa maana ulinijaza hasira yako.


Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi.


“Kama ndugu yako akikukosea, umwendee kwa kumwonyesha kosa lake, mukiwa ninyi wawili peke yenu. Na kama akikusikia, unarudiliana na ndugu yako.


Yoane alimukaripia mutawala Herode juu ya kumwoa Herodia, muke wa ndugu yake Filipo na juu ya mabaya mengine.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Usiku umepita, na muchana unakaribia. Basi tutupilie mbali matendo ya giza na kuvaa silaha za kupigana nazo wakati wa mwangaza.


Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!


Anayepanda kwa kupendeza hali yake ya kimwili, atavuna matunda yanayotokana na hali ile, nayo ni lufu. Lakini anayepanda kwa kupendeza Roho Mutakatifu, atavuna matunda yanayotokana na Roho yule, nayo ni uzima wa milele.


Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.


(Kwa maana ni haya kusema juu ya mambo watu hao wanayofanya kwa siri.)


mumushukuru Mungu Baba aliyewawezesha ninyi kuwa wenye kustahili kupokea sehemu yenu ya urizi aliowawekea watu wake katika ufalme wa mwangaza.


Kwa maana wale wanaolala usingizi wanalala usiku, na wale wanaolewa, wanalewa usiku.


Kama mutu hataki kushika maagizo tunayowatolea katika barua hii, mumwangalie vizuri mutu yule, musishirikiane naye, kusudi apate haya.


Wandugu, tunawaagiza katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba mujitenge na wandugu wote wanaokuwa wavivu na wasiofuata mafundisho tuliyowapa.


Wale wenye kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watu kusudi wengine wapate kuogopa vilevile.


Usiweke mikono juu ya mutu kwa haraka, wala usishiriki zambi za watu wengine. Ujilinde wewe mwenyewe katika maisha safi.


na magomvi yasiyokuwa na mwisho ya watu wenye akili iliyokwisha kupotoka hata wamesahau ukweli kabisa. Ndio wale wanaozani kwamba dini ni njia ya kupata utajiri.


Kwa inje watajionyesha kama watu wenye kushikamana na ibada, lakini wanazarau uwezo wake. Ujiepushe na watu hao.


utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.


Haya ndiyo maneno unayopaswa kufundisha, ukiwaonya watu na kuwakaripia kwa mamlaka yote. Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote.


Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ