Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 4:2
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, ingawa wewe uko juu ya wote, unawaangalia wanyenyekevu kwa wema; lakini, unatambua wenye kiburi kwa mbali.


Ujifungie upanga wako, ewe shujaa! Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka.


Afazali kuwa munyenyekevu pamoja na masikini, kuliko kugawanyana vitu vya unyanganyi pamoja na wenye kiburi.


Yeye anazarau wenye mazarau, lakini anakubali wanyenyekevu.


Mwisho wa jambo ni afazali kuliko mwanzo wake. Moyo muvumilivu ni bora kuliko moyo wa majivuno.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


(Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)


Mukubali kuongozwa nami kama vile ngombe dume anayefungiwa nira, nanyi mufuate mafundisho yangu maana mimi ni mupole na munyenyekevu. Kwa hiyo mutapumzika.


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Nilimutumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi na katika majaribu niliyopata kwa ajili ya mashauri mabaya Wayuda waliyonifanyia.


Sisi tunaokuwa na nguvu katika imani tunapaswa kubeba muzigo wa uzaifu wa wale wasiokuwa na nguvu. Tusifanye tu mambo yanayotupendeza wenyewe.


Upendo hauchoki na mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote na kuvumilia mambo yote.


Musaidiane ninyi kubeba mizigo yenu, na hivi mutatimiza sheria ya Kristo.


Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,


Mungu atawatia nguvu kwa uwezo wake wenye utukufu, kusudi mupate kuvumilia kila kitu pasipo kuchoka. Basi kwa furaha,


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Kwa sababu hiyo, mutupilie mbali mambo yote machafu na matendo ya uovu yanayozidi. Mupokee kwa unyenyekevu neno lile lililopandwa ndani yenu na linaloweza kuwaokoa.


Lakini mumutukuze Bwana wenu Kristo ndani ya mioyo yenu. Mukuwe tayari wakati wowote kumujibu kila mutu anayewauliza juu ya tumaini munalokuwa nalo. Lakini mufanye vile kwa upole na heshima,


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ