Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kwa uongozi wake, viungo vyote vya mwili vinashikamana kabisa, nao mwili wote muzima unashikamana vizuri kwa nguvu ya maunganio yake. Halafu, kila kiungo kinapotumika kama kinavyopaswa, mwili wote unakomaa na kujijenga katika upendo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 4:16
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Mimi ni muzabibu, nanyi ni matawi. Anayekaa ndani yangu, na mimi ndani yake anazaa matunda mengi, kwa sababu pasipo mimi hamuwezi kufanya kitu.


Katika mwili mumoja kuna viungo vingi, lakini viungo hivi vyote havina kazi moja.


Kwa kuwa mukate ni mumoja, ijapokuwa sisi ni wengi, tuko mwili mumoja, kwa maana sisi wote tunashiriki mukate ule mumoja.


Basi sasa, hivi vitu vitatu vinadumu: imani, tumaini na upendo; lakini kinachokuwa kikubwa kuliko hivi vingine ni upendo.


Sasa tuangalie mambo yanayoelekea nyama zinazotolewa kwa kutambikia sanamu za miungu: tunajua kwamba “sisi wote tuko na elimu,” kama vile munavyozoea kusema. Elimu inamufanya mutu kuwa na kiburi, lakini upendo unawajenga watu katika imani.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Nimewekwa kuwa mutumishi wa Habari Njema kwa njia ya zawadi Mungu aliyonipatia kutokana na uwezo wake.


Yeye amefanya vile kwa kuwatayarisha watu wa Mungu kwa kazi ya utumishi kusudi mwili wa Kristo upate kujengwa.


Lakini tukitangaza ukweli kwa upendo, tutakomaa katika mambo yote na kufikia kuwa kama Kristo, ambaye ni kichwa.


Na kitu ninachoomba kwa Mungu, ni kwamba upendo wenu uzidi kuongezeka katika ufahamu wa kweli na usikilivu kamili,


Mutu yule hashikamani na Kristo anayekuwa kichwa cha mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili muzima unakulishwa vizuri na kuunganishwa pamoja kwa njia ya maunganio na vifundo vyake, kusudi upate kukomaa kufuatana na mapenzi ya Mungu.


Ninapigana kusudi wapate kuwa na bidii na kuungana katika upendo. Na zaidi ya hii wapate kuwa na uhakika kabisa unaotokana na ufahamu mukamilifu. Hivi wataweza kujua siri ya Mungu, maana yake kumujua Kristo mwenyewe,


Kwa maana tunakumbuka mbele ya Mungu Baba yetu namna munavyotumika kwa imani na munavyojisumbua na kazi kwa ajili ya upendo wenu. Vilevile tunakumbuka namna tumaini lenu katika Yesu Kristo linavyokuwa imara.


Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.


Na Bwana awaongezee na kuwazidishia upendo munaokuwa nao ninyi kwa ninyi na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tunavyowapenda ninyi.


Wandugu, tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu. Inatufaa kufanya vile kwa maana imani yenu inaongezeka, nao upendo wenu ninyi kwa ninyi unazidi kuongezeka.


Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Na sisi tumejua na kuamini upendo Mungu anaokuwa nao kwetu. Mungu ni upendo. Yule anayeishi katika upendo anaungana na Mungu, na Mungu anaungana naye.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ