Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yeye amefanya vile kwa kuwatayarisha watu wa Mungu kwa kazi ya utumishi kusudi mwili wa Kristo upate kujengwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 4:12
45 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


Yuda alikuwa mumoja wa kundi letu, naye alikuwa ameshiriki pamoja nasi katika kazi hii.”


kusudi atiwe katika kazi hii ya kuwa mutume kwenye nafasi Yuda aliyoacha na kwenda pahali pake mwenyewe.”


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.


Hivi vilevile, sisi tunaokuwa wengi tumekuwa mwili mumoja katika kuungana kwetu na Kristo, na sisi wote ni viungo kila mumoja kwa mwingine.


Aliyepewa zawadi ya utumishi, atumike. Aliyepewa zawadi ya kufundisha, afundishe.


Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.


Wandugu zangu, kwa ngambo yangu ninajua hakika kwamba ninyi munajaa wema, nanyi munafahamu yote yanayofaa na munaweza kushauriana vizuri.


Lakini kila mumoja wetu anapaswa kumupendeza mwingine kwa kumutendea mema na kuweza hivi kumujenga katika imani.


Nami ninajua kwamba wakati nitakapokuja kwenu, nitakuja na baraka nyingi sana kutoka kwa Kristo.


Ninyi wote ni mwili wa Kristo, na kila mumoja wenu ni kiungo cha mwili ule.


Na kwa kila mutu Roho anajifunua kwa faida ya wote.


Hivi vilevile kufuatana na vile munavyotamani sana zawadi za Roho, mujikaze kupata kwa uwingi zile zinazoweza kujenga kanisa katika imani.


Kwa maana kama nikiomba katika luga ya ajabu, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haitumiki.


Wandugu zangu, niseme nini basi? Wakati munapokusanyika kwa ibada, mumoja anaweza kuimba wimbo, mwingine kufundisha, mwingine kutoa ufunuo, mwingine kusema kwa luga za ajabu na mwingine anaweza kutafsiri. Na hayo yote yanapaswa kufanyika katika nia ya kujenga kanisa katika imani.


Ninyi munazani kwamba kwa wakati huu wote sisi tunajitetea mbele yenu? Tunasema mambo yale mbele ya Mungu kufuatana na vile tunavyoungana na Kristo. Wandugu wapendwa, mambo yale yote ni kwa kuwajenga ninyi katika imani.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Tunafurahi wakati ninyi munapokuwa na nguvu, hata ikiwa sisi ni zaifu. Nasi tunawaombea kusudi mupate kuwa wakamilifu.


Basi si zaidi sana matokeo ya utumishi wa Roho yatakuwa yenye utukufu?


Kwa wema wake, Mungu ametupatia utumishi huu, na kwa sababu hii sisi hatukati tumaini.


Mambo haya yote yalifanyika na Mungu, aliyetupatanisha naye kwa njia ya Kristo na kutupatia kazi ya kuongoza watu wengine wapatane naye.


Sisi hatutaki kumukwaza mutu yeyote katika jambo lolote kusudi kazi yetu isizarauliwe.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Kanisa ni mwili wa Kristo, nalo ni utimilifu wa Kristo anayetimiza vitu vyote.


Kwa uongozi wake, viungo vyote vya mwili vinashikamana kabisa, nao mwili wote muzima unashikamana vizuri kwa nguvu ya maunganio yake. Halafu, kila kiungo kinapotumika kama kinavyopaswa, mwili wote unakomaa na kujijenga katika upendo.


Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.


Kuna mwili mumoja na Roho mumoja, vilevile kuna tumaini moja la mwito muliotolewa na Mungu.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Ni kwa hiyo tunamutangaza Kristo kwa watu wote. Tunaonya na kufundisha kila mutu kwa hekima yote, kusudi tuwasaidie watu wote wapate kufikia kuwa wakamilifu katika kuungana kwao na Kristo.


Mumwambie Arkipo aangalie vizuri atimize kazi ile aliyopewa na Bwana.


Ninamushukuru Bwana wetu Kristo Yesu aliyenitia nguvu, kwa sababu alinihesabu kuwa mwaminifu hata akaniweka kwa kazi yake.


Luka peke yake ndiye anayekuwa hapa pamoja nami. Umutwae Marko, ukuje pamoja naye, kwa sababu ananifalia katika kazi yangu.


Lakini wewe, ujiangalie katika mambo yote, uvumilie mateso, ufanye kazi yako ya kuhubiri Habari Njema na kutimiza kabisa utumishi wako.


Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Basi kwa sababu hii, tuache mafundisho ya mwanzo juu ya Kristo. Tusijenge tena musingi mupya wa mambo haya: kugeuka toka katika matendo yasiyofaa, kumwamini Mungu, namna mbalimbali za ubatizo, kuwawekea watu mikono, ufufuko na hukumu ya milele. Tuendelee katika mafundisho makamilifu. Tutafanya hivi, Mungu akitaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ