Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 3:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kwa hiyo ninyi pamoja na watu wote wa Mungu mutaweza kutambua katika ngambo zote ukubwa wa upendo wa Kristo unaopita kipimo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 3:18
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Sasa, ee Yawe, Mungu, uingie pahali pako pa kupumzika, wewe pamoja na Sanduku la Agano la nguvu zako. “Ee Yawe, Mungu, makuhani wako wapate wokovu, na watakatifu wako wafurahie uzuri wako.


Lakini wema wa Yawe unadumu milele, kwa wale wote wanaomwabudu; na haki yake inadumu vizazi vyote,


Kifo cha waaminifu wa Yawe si jambo dogo mbele yake.


Makuhani wako wakuwe watu wa haki siku zote; na waaminifu wako wapige vigelegele vya furaha!


Ufahamu wako unapita akili yangu; ni mukubwa sana, siwezi kuuelewa.


Viumbe vyako vyote vitakushukuru, ee Yawe, nao waaminifu wako watakutukuza.


Kama vile mbingu zinavyokuwa mbali na dunia, ndivyo njia zangu zinavyokuwa mbali na zenu, na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Hakuna anayekuwa na upendo mukubwa kuliko mutu anayetoa maisha yake kwa ajili ya warafiki zake.


Hawakufahamu namna Mungu anavyowahesabia watu haki na wakatafuta kusimamisha haki yao wenyewe. Wakakataa kufuata njia ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu na ushirika wa Roho Mutakatifu.


Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia namna munavyomwamini Bwana Yesu na namna munavyowapenda watu wote wa Mungu,


Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa.


Hayo yote ni kwa maana tumesikia namna munavyomwamini Yesu Kristo na namna munavyowapenda watu wote wa Mungu.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ