Lakini mbele mambo hayo yote yatokee, mutakamatwa na kuteswa. Watawapeleka kwenda kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia na kuwatia katika vifungo. Vilevile mutapelekwa mbele ya wafalme na ya wakubwa kwa ajili ya jina langu,
Yule mukubwa akaenda pamoja naye kwa jemadari na kumwambia: “Yule mufungwa Paulo aliniita, akaniomba nikuletee kijana huyu kwa sababu yuko na neno la kukuambia.”
Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”
Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.
Kama sisi tunapata taabu ni kusudi mupate kufarijiwa na kuokolewa. Kama tunafarijiwa ninyi vilevile munafarijiwa na kupata nguvu ya kuwawezesha kuvumilia taabu ile ile tunayopata.
Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.
Sasa nitasema kama mwenda-wazimu: wao ni watumishi wa Kristo? Mimi ni mutumishi wake zaidi kuliko wao. Nimetumika kazi nyingi zaidi, nimefungwa mara nyingi zaidi, nimepigwa zaidi, na mara nyingi nimekuwa katika hatari ya kufa.
Wandugu, ikiwa mimi ningali ninahubiri ya kama ni lazima kutahiriwa, basi kwa sababu gani ningali ninateswa? Kama ningefanya vile, basi watu hawangechukizwa na mahubiri yangu juu ya musalaba wa Kristo.
Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.
Mimi ni mujumbe wa Habari ile Njema, ijapokuwa sasa ninakuwa katika kifungo. Basi muniombee kusudi nipate kusema kwa uhodari, sawa inavyonipasa kusema.
Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.
Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.
Mimi Paulo ninawatumia salamu zangu, nikiziandika kwa mukono wangu mwenyewe. Musisahau kwamba mimi ningali katika kifungo. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.
Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.
Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo, na kwa ndugu yetu Timoteo. Tunakuandikia wewe Filemono, mupendwa wetu na mwenzetu wa kazi,
Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.