Kwa hiyo ahadi inafuatana na imani, kusudi ikuwe imetolewa kwa neema ya Mungu. Na zaidi kuwe uhakikisho kwamba ahadi hiyo ni kwa ajili ya wazao wote wa Abrahamu, si kwa wale wanaotii Sheria tu, lakini vilevile kwa wale wanaokuwa na imani kama Abrahamu, babu yetu sisi wote.
Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.
Kwa maana yote yanayoonekana wazi yanageuka mwangaza. Ni kwa hiyo inasemwa hivi: “Amuka wewe unayelala! Ufufuke kutoka kati ya wafu, naye Kristo atakuangazia.”
Zamani mulikuwa mumekufa kwa sababu ya zambi zenu na kwa sababu mulikuwa watu wa mataifa mengine, wasiotahiriwa. Lakini sasa, Mungu amewapatia ninyi uzima pamoja na Kristo, naye ametusamehe zambi zetu zote.
alituokoa sisi. Hakufanya vile kwa sababu ya matendo yetu ya haki, lakini alituokoa kwa sababu ya huruma yake kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetuwezesha kuzaliwa mara ya pili na kuwa na maisha mapya kwa kutusafisha kwa maji.