Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Zamani, sisi wote vilevile tulikuwa kama wao. Tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kimwili na kutenda kufuatana na mapenzi ya mwili na roho zetu. Kwa sababu ya hali yetu ya kimwili, hatungeponyoka kasirani ya Mungu kama wengine.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 2:3
54 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Adamu alipokuwa na umri wa miaka mia moja na makumi tatu, alipata mutoto aliyefanana naye, na mwenye sura kama yake; akamwita Seti.


Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


lakini masumbuko ya dunia hii, udanganyifu wa mali, na tamaa za namna nyingine vikiwaingia, vinasonga lile Neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Hawakuzaliwa kuwa watoto wa Mungu kwa namna ya kimutu, wala kwa mapenzi ya kimwili, wala kwa mapenzi ya mutu, lakini wamezaliwa na Mungu.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Katika siku zilizopita Mungu aliwaachilia watu wa mataifa yote wafuate njia wanazotaka.


Kwa sababu hii Mungu aliwaacha wajichafue wenyewe kwa kufuata tamaa ya mioyo yao na kutendeana mambo ya haya wao kwa wao.


Zamani ninyi mulimwasi Mungu, lakini sasa amewahurumia kutokana na uasi wa Wayuda.


Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.


Watu wa mataifa hawana Sheria ya Musa. Lakini wanapofanya sawa inavyoamuriwa na Sheria ile kutokana na zamiri yao, wao ni Sheria kwa ajili yao wenyewe, ijapokuwa hawana Sheria ile.


Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.


Sasa kwa kuwa tumehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya damu ya Yesu, inaonyesha zaidi sana kwamba atatuokoa kusudi kasirani ya Mungu isituangukie.


Basi musiache tena zambi kutawala katika mwili wenu wa kufa, hata mupate kufuata tamaa zake mbaya.


Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.


Basi kuna nini? Mungu alitaka kuonyesha kasirani yake na kutambulisha uwezo wake. Lakini aliwavumilia sana wale waliostahili kupatwa na kasirani yake na waliokuwa wametayarishwa kwa kuangamizwa.


Ni nani aliyekuweka kuwa mukubwa kuliko wengine? Si Mungu ndiye aliyekupa vitu vyote unavyokuwa navyo? Ikiwa ni hivi, kwa sababu gani unajivuna kama vile haukuvipewa kama zawadi?


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Lakini Maandiko Matakatifu yanasema kwamba watu wote wako chini ya utumwa wa zambi, kusudi zawadi iliyoahidiwa na Mungu itolewe kwa wale wanaoamini kwa njia ya imani yao katika Yesu Kristo.


Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.


Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.


Na ninyi zamani mulikuwa mbali na Mungu, mulikuwa waadui zake kwa sababu ya mafikiri na matendo yenu mabaya.


Wandugu, hatutaki mukose kujua habari zinazowaelekea wale waliokufa, kusudi musikuwe na huzuni sawa vile watu wasiokuwa na tumaini la kufufuka.


Basi tusilale usingizi kama vile wengine, lakini tukeshe na kuwa wakadirifu.


Lakini wale wanaotaka kuwa watajiri wanaanguka katika majaribu na mitego, na katika tamaa nyingi za upumbafu na mabaya zinazowatumbukiza katika anguko na uharibifu.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Kama watoto wenye utii, musiachilie maisha yenu kutawaliwa na tamaa mbaya mulizokuwa nazo zamani wakati mulipokuwa mukiishi katika ujinga.


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.


Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.


Kwa ngambo ingine amri hii ninayowaandikia ni mupya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu vilevile. Kwa maana giza linapita na mwangaza wa kweli umekwisha kutokea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ