Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 2:2
64 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Umeme wa radi umewachoma na kuwateketeza kondoo na watumishi. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Mara moja upepo mukali ukavuma kutoka katika jangwa, ukaipiga nyumba ile kila upande nayo ikawaangukia, na vijana wote wamekufa. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Yawe akamwuliza Shetani: “Unatoka wapi wewe?” Shetani akamujibu Yawe: “Ninatoka kutembeatembea na kuzungukazunguka katika dunia.”


kama hatua zangu zimepotoka nao moyo wangu ukafuata tamaa za macho yangu, kama mikono yangu imechafuliwa na zambi,


Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Ni nani munayemuchekelea? Munamuzomea nani na kumutoshea ulimi inje? Ninyi wenyewe ni waasi tangu mwanzo, ninyi ni kizazi kidanganyifu.


Maana, inchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya laana, inchi inaomboleza, na mashamba ya kulishia nyama yamekauka. Mienendo ya watu ni miovu, wanapoteza nguvu kwa ajili ya mambo yasiokuwa ya haki.


Enyi Waisraeli, ninyi mumetenda zambi tangia kule Gibea, na mpaka sasa munaendelea. Hakika vita itawaangamizia kulekule Gibea.


mbuni, kirukanjia, dudumizi, aina zote za kipanga,


Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Shamba ni dunia. Mbegu nzuri ni washiriki wa Ufalme. Nyasi ni washiriki wa yule Mwovu Shetani.


lakini masumbuko ya dunia hii, udanganyifu wa mali, na tamaa za namna nyingine vikiwaingia, vinasonga lile Neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Basi bwana wa yule mulinzi akamusifu kwa sababu alitenda kwa werevu. Kwa maana watu wa dunia hii wanatengeneza maneno yao na wenzao kwa werevu sana kuliko watu wanaopenda kuishi katika mwangaza.”


“Simoni, Simoni! Sikiliza: Shetani ameachiliwa wakati wa kuwajaribu na kuwatenga kabisa.


Sasa ni wakati wa dunia hii kuhukumiwa; sasa mutawala wa dunia hii atashindwa.


Wakati Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakikula chakula cha magaribi, Shetani alikuwa amekwisha kumushawishi Yuda mwana wa Simoni Iskariota kwamba amutoe Yesu.


Yuda alipokwisha kukamata kile kipande cha mukate, Shetani akamwingilia. Basi Yesu akamwambia: “Unayotaka kufanya, uyafanye upesi!”


Sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa sababu mutawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu,


Kama mungekuwa watu wa dunia, dunia ingewapenda, kwa maana ninyi ni watu wake. Lakini nimewachagua ninyi toka dunia hii, na ninyi si watu wa dunia tena. Ni kwa sababu hii dunia inawachukia.


Na kuelekea hukumu ni kwa sababu mutawala wa dunia hii amekwisha kuhukumiwa.


Watu wa dunia hawawezi kuwachukia ninyi, lakini wananichukia mimi kwa sababu ninashuhudia kwamba matendo yao ni mabaya.


Yesu akawajibu: “Ninyi munatoka hapa chini, lakini mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa dunia hii, lakini mimi si wa dunia hii.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Kwa mwisho katibu mukubwa wa muji akawatuliza watu, akisema: “Ninyi wanainchi wenzangu wa Efeso, watu wote wanajua kwamba ni wakaaji wa Efeso ndio wanaoshugulika na kulinda hekalu la mungu Artemi na sanamu yake iliyoshuka toka mbinguni.


Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Hiyo sikusema kabisa kwamba musishirikiane na wote wanaokuwa wazinzi katika dunia hii, wala wenye tamaa, wala wanyanganyi, wala wenye kuabudu sanamu. Kwa maana kwa kujitenga nao, ingewapasa kutoka katika dunia!


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.


Na kule anatawala juu ya wakubwa wote, wenye mamlaka wote, wenye uwezo wote na wasultani wote na juu ya kila cheo kinachoweza kuwa katika dunia hii na katika dunia itakayokuja.


Basi mukumbuke namna mulivyokuwa zamani ninyi munaokuwa kwa kizalikio watu wa mataifa mengine. Wayuda wanawaita ninyi watu wasiotahiriwa, lakini wao wanajiita wenye kutahiriwa kwa sababu ya kitambulisho cha kutahiriwa na watu katika miili yao.


Lakini sasa, katika kuungana kwenu na Yesu Kristo, ninyi muliokuwa mbali, mumekuwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.


Zamani, sisi wote vilevile tulikuwa kama wao. Tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kimwili na kutenda kufuatana na mapenzi ya mwili na roho zetu. Kwa sababu ya hali yetu ya kimwili, hatungeponyoka kasirani ya Mungu kama wengine.


Basi, kwa jina la Bwana ninawaonya hivi: musiishi tena kama watu wa mataifa mengine, wanaofuata mawazo yao ya bure


Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.


Mutu asiwadanganye na maneno yasiyokuwa na maana; kwa sababu ya makosa kama hayo, Mungu anawaazibu kwa kasirani yake wale wasiomutii.


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.


Na ninyi zamani mulikuwa mbali na Mungu, mulikuwa waadui zake kwa sababu ya mafikiri na matendo yenu mabaya.


Dema amependelea mambo ya dunia hii akaniacha na kwenda Tesalonika. Kreske akaenda Galatia, na Tito akaenda Dalmatia.


Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.


Mutu wa namna hiyo asizani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Bwana,


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


Kama watoto wenye utii, musiachilie maisha yenu kutawaliwa na tamaa mbaya mulizokuwa nazo zamani wakati mulipokuwa mukiishi katika ujinga.


Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.


Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


kwa sababu kila mutoto wa Mungu anashinda dunia. Tunashinda dunia kwa njia ya imani yetu.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Akawadanganya wakaaji wa dunia kwa njia ya vitambulisho alivyowezeshwa kuonyesha mbele ya yule nyama mukubwa wa kwanza. Aliwaambia watu wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule nyama aliyeumizwa kwa upanga, lakini aliendelea kuishi.


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


Malaika wa saba akamwanga kikombe chake katika anga. Halafu sauti kubwa ikasikilika kutoka katika hekalu kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa ni mwisho!”


Akamukamata yule nyoka mukubwa, ndiye yule nyoka wa zamani, anayeitwa “Mwovu” au “Shetani” na kumufunga kwa muda wa miaka elfu moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ