Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 akitupatia hekima na akili kamili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 1:8
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, matendo yako ni mengi sana! Umeyafanya kwa hekima yote! Dunia imejaa viumbe vyako!


Mimi Hekima nina ujuzi; nina maarifa na akili.


Mungu anasema hivi: Mutumishi wangu atafanikiwa; atatukuzwa na kupewa cheo, atapata heshima kubwa.


Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Lakini kuna tofauti kubwa kati ya zawadi ya Mungu na kosa la Adamu. Kwa maana ikiwa kosa la mutu mumoja lilisababisha kifo cha watu wengi, inaonyesha zaidi sana kwamba Mungu amezidisha neema yake kwa ajili ya watu wengi na zawadi inayotokana nayo kwa njia ya mutu mumoja, Yesu Kristo.


Ninatangaza hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichwa kwa watu, na iliyopangwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia kwa ajili ya utukufu wetu.


Mungu amefanya kila kitu kufuatana na kusudi na mapenzi yake. Yeye ametuchagua kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watu wake.


Kwa njia ya damu ya Kristo, sisi tumekombolewa, maana yake zambi zetu zimesamehewa. Hivi Mungu ameonyesha uwingi wa neema yake


Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.


yeye anayekuwa Mungu peke yake, Mwokozi wetu, asifiwe na kuwa na ukubwa, uwezo na mamlaka, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu, tangia zamani za kale, sasa na hata milele! Amina.


Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ