Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waefeso 1:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Kanisa ni mwili wa Kristo, nalo ni utimilifu wa Kristo anayetimiza vitu vyote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waefeso 1:23
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sisi wote tumepokea sehemu ya neema aliyojaa nayo, akitupatia baraka nyingi sana.


Kwa sababu hii ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa azabu ya Mungu tu, lakini tena kwa sababu ya kusongwa na zamiri.


Kuna kazi za namna mbalimbali, lakini Mungu ni mumoja anayewezesha watu wote kuzitimiza.


Na wakati vitu vyote vitakapokuwa vimewekwa chini ya mamlaka ya Mwana, halafu yeye mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Mungu aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote, kusudi Mungu apate kutawala juu ya vyote kabisa.


Kristo alivunja uadui kwa njia ya kufa kwake juu ya musalaba, akaunganisha watu wa makabila haya mawili kuwa moja na kuwapatanisha na Mungu.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa.


Yule aliyeshuka ndiye yule yule aliyepanda juu sana kupita mbingu zote kusudi akamilike katika ulimwengu wote.


Yeye amefanya vile kwa kuwatayarisha watu wa Mungu kwa kazi ya utumishi kusudi mwili wa Kristo upate kujengwa.


Hivi, sisi wote tutafikia umoja wa imani yetu na wa kumujua kabisa Mwana wa Mungu; tutapata kukomaa na kufikia kipimo cha utimilifu wa Kristo.


Kuna mwili mumoja na Roho mumoja, vilevile kuna tumaini moja la mwito muliotolewa na Mungu.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Mutu yule hashikamani na Kristo anayekuwa kichwa cha mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili muzima unakulishwa vizuri na kuunganishwa pamoja kwa njia ya maunganio na vifundo vyake, kusudi upate kukomaa kufuatana na mapenzi ya Mungu.


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu; maana ni kwa ajili ya hiyo ninyi mumeitwa kuwa katika mwili mumoja. Mukuwe wenye shukrani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ