Chumba cha ndani, kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana, kilijengwa katika sehemu ya nyuma ya nyumba. Kilikuwa kimejengwa kwa mbao za mierezi kutokea kwenye sakafu mpaka kwenye dari, na urefu wake ulikuwa metre tisa.
Kisha makuhani wakaliingiza Sanduku la Agano la Yawe kwa nafasi yake katika chumba cha ndani cha nyumba, ni kusema Pahali Patakatifu Sana, chini ya mabawa ya makerubi.
Akakipima chumba chenyewe, nacho kilikuwa cha muraba pande zake zikiwa na upana wa metre kumi. Chumba hiki kilikuwa mbele ya baraza la katikati. Kisha, akaniambia: Hapa ndipo Pahali Patakatifu Sana.
Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wana wake wataingia katika hema, na kushusha pazia linalokuwa mbele ya Sanduku la Agano, kisha walifunike kwa pazia hilo.
Tumaini hili linasimamisha imara na kulinda mioyo yetu kama vile nanga inavyosimamisha mashua imara. Nalo linapita katika pazia na kuingia katika Pahali Patakatifu Sana.
Lakini ni Kuhani Mukubwa peke yake ndiye aliyeingia katika kile chumba cha pili mara moja tu kila mwaka. Naye alipaswa kupeleka mule damu ya nyama anayotoa sadaka kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kwa ajili ya zambi watu walizofanya kwa kutokujua.
Hivi Roho Mutakatifu alikuwa akionyesha kwamba njia ya kuingia katika Pahali Patakatifu Sana ilikuwa bado kufunguliwa kwa wakati wote ile Hema ya kwanza ilipokuwa ingali ikisimikwa.