Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 9:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 9:28
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Kwa nini hamukumukula katika Pahali Patakatifu kwa vile huyo ni kitu kitakatifu kabisa na mulikuwa mumepewa huyo kwa kuondoa kosa ya Waisraeli wote pamoja na kuwafanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe?


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Basi, Yawe akamwambia Haruni: Wewe na wana wako na ukoo wako mutabeba lazima ya kazi za hema takatifu; vilevile na makosa yanayoambatana na ukuhani wako wewe mwenyewe na wana wako.


Lakini Walawi peke yao ndio watakaotumika katika hema la mukutano; na kuwa na mapaswa kwa ukamilifu juu yake. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu vyote. Walawi hawatakuwa na mali ya kurizi katika inchi ya Israeli,


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.


kwa maana hii ni damu yangu inayomwangika kwa ajili ya wengi kusudi wasamehewe zambi. Nayo damu hii inahakikisha agano la Mungu.


Nami nitakapokwisha kuwatayarishia ninyi nafasi, nitarudi tena na kuja kuwatwaa, kusudi pahali nitakapokuwa, ninyi mupate kuwa pale vilevile.


Watu hao wakawaambia: “Ninyi Wagalilaya, sababu gani munasimama pale mukiangalia mbinguni? Huyu Yesu aliyenyanyuliwa toka katikati yenu kwenda mbinguni, atarudi sawa vile mulivyomwona akienda.”


Kristo alitolewa na Mungu kuwa sadaka ya usamehe wa zambi kwa njia ya damu yake kwa ajili ya wenye kumwamini. Mungu alifanya hivi kwa kuonyesha haki yake. Zamani, katika uvumilivu wake, aliacha kuazibu zambi za watu. Lakini kwa wakati wa sasa anaonyesha haki yake kusudi akuwe mwenye haki na kumuhesabia haki kila mutu anayemwamini Yesu.


Lakini kuna tofauti kubwa kati ya zawadi ya Mungu na kosa la Adamu. Kwa maana ikiwa kosa la mutu mumoja lilisababisha kifo cha watu wengi, inaonyesha zaidi sana kwamba Mungu amezidisha neema yake kwa ajili ya watu wengi na zawadi inayotokana nayo kwa njia ya mutu mumoja, Yesu Kristo.


Kuelekea jambo la kufa kwake, alikufa mara moja tu kwa ajili ya zambi; lakini kuelekea maisha yake, sasa anaishi kwa ajili ya Mungu.


Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


hata hamukosewi zawadi yoyote ya Mungu, mukiwa mukingojea wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapoonekana.


Na wakati mwili huu wa kuharibika utakapovaa ule wa kutoharibika, nao mwili wa kufa utakapovaa ule wa kutokufa, halafu Maandiko Matakatifu haya yatatimia: “Kifo kimekomeshwa; kimeshindwa kabisa.”


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Sasa tunawaandikia juu ya mambo yanayoelekea kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo na namna sisi tutakavyokusanyika mbele yake. Wandugu, tunawasihi sana,


Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Na kwa sababu Yesu Kristo alifanya mapenzi ya Mungu, sisi tumetakaswa zambi kwa njia ya mwili wake alioutoa sadaka kwa mara moja tu.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.


Yeye hahitaji kutoa sadaka kila siku kama vile Makuhani wengine Wakubwa, kwanza kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kisha kwa ajili ya zambi za watu. Kwa maana amefanya vile mara moja tu wakati alipojitoa mwenyewe kufa.


Kuhani Mukubwa wa Wayuda anaingia katika Pahali Patakatifu Sana kila mwaka, akibeba damu ya nyama. Lakini Kristo hakuingia humo kusudi ajitoe mwenyewe sadaka mara nyingi.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


mukingojea na kuharikisha kuja kwa Siku ile ya Mungu; ndiyo siku mbingu zitakapoyeyushwa kwa moto, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitakapoyeyuka.


Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.


Ninyi munajua kwamba Yesu Kristo alikuja kusudi aondoe zambi, na hakuna zambi ndani yake.


Mudumu katika upendo wa Mungu, mukimungojea Bwana wetu Yesu Kristo, atakayewapa ninyi uzima wa milele kwa huruma yake.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ