Nawe utamuchinja na kutwaa sehemu ya damu na kumupakaa Haruni na wana wake kwenye incha za masikio yao ya kuume na vidole gumba vya mikono yao ya kuume, na vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Damu inayobaki utairushia juu ya mazabahu pande zake zote.
na kila siku utatoa ngombe dume akuwe sadaka ya maondoleo ya zambi kwa kufanya upatanisho. Kwa kufanya hivyo utasafisha mazabahu, kisha utaimiminia mafuta kwa kuitakasa.
Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.
Halafu Haruni akamuchinja vilevile ngombe dume na yule kondoo dume wa sadaka za amani kwa ajili ya watu. Wana wake wakamuletea damu ambayo aliinyunyizia mazabahu pande zote.