17 Agano kama hili linatimizwa nyuma ya kifo cha yule aliyelifanya, lakini si wakati angali muzima.
Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Kama vile unavyoona, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisha katika inchi ya babu zenu.
“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.
Wandugu, nitatumia mufano huu wa kawaida: mutu anapofanya agano kwa njia ya haki, hakuna mutu anayeweza kulivunja au kuongeza neno lingine juu yake.
Katika mambo yenye kuelekea agano la urizi, ni lazima kuhakikisha kwamba yule aliyelifanya amekwisha kufa.
Kwa sababu hii, hata lile agano la kwanza halikuwekwa pasipo kumwangika kwa damu.