Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 8:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alimupatia mufano wa yote aliyokusudia ndani ya moyo juu ya viwanja vya nyumba ya Yawe, vyumba vya Mungu na gala za kuwekea vitu vitakatifu.


Hayo yote, mufalme Daudi aliyaweka wazi kwa maandiko aliyopewa na Yawe. Kazi yote itendeke kulingana na mufano ule.


Hakikisha kwamba umevitengeneza kwa mufano ulioonyeshwa kule juu ya mulima.


Utatengeneza hema hiyo na vifaa vyake kulingana na mufano nitakaokuonyesha.


Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mufano niliokuonyesha juu ya mulima.


Utatengeneza mazabahu kwa mbao, ikuwe wazi ndani, kulingana na mufano niliokuonyesha juu ya mulima.


Toka sehemu za juu mpaka chini kinara hicho cha taa kilikuwa kimetengenezwa kwa ufundi mukubwa kwa zahabu iliyofuliwa kufuatana na mufano ambao Yawe alikuwa amemwonyesha Musa.


Nyuma ya maneno haya, Mungu akawaonya katika ndoto kwamba wasirudie tena kwa Herode, kisha wakarudia katika inchi yao wakipitia njia nyingine.


“Kule katika jangwa babu zetu walikuwa na ile hema inayokuwa na vibao vya agano ndani yake. Hema ile ilikuwa imetengenezwa kama vile Mungu alivyomwagiza Musa, na mufano ule alioonyeshwa.


Mambo hayo yote ni kivuli cha mambo yatakayokuja, lakini ukweli wa mambo yote ni Kristo mwenyewe.


Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.


Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Sisi tuko na mazabahu yetu, nao makuhani Wayuda wanaotumika katika Pahali Patakatifu hawana ruhusa ya kula sehemu ya vitu vinavyotolewa sadaka juu ya mazabahu ile.


Huo ni mufano wa wakati wa sasa unaoonyesha kwamba matoleo na sadaka zinazotolewa kwa Mungu haziwezi kumufanya yule anayeabudu kuwa na moyo mukamilifu.


Tena tulifikiri kwamba ikiwa jambo kama hilo litasemwa juu yetu au juu ya wazao wetu katika siku zinazokuja, tutasema: ‘Muangalie mufano wa mazabahu ya Yawe ambayo wazee wetu waliijenga; sio kwa ajili ya kutolea juu yake sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka zingine lakini kama ushuhuda kati yetu na ninyi’.


Na nyuma ya pale nikaona hekalu limefunguliwa mbinguni; mule mulikuwa hema yenye vibao vya agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ