4 Basi muangalie namna mutu huyu alivyokuwa mukubwa, hata babu yetu mukubwa Abrahamu alimupa fungu moja la kumi la vitu vyote alivyoteka katika vita.
Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.
Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.
“Wandugu, inanipasa kuwaambia kwa uhodari juu ya babu yetu mukubwa Daudi. Yeye alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lingali hata leo.
Na maandiko haya yakatimia: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.” Na Mungu akamwita rafiki yake.