Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 naye Abrahamu akamupa fungu moja la kumi la vitu vyote alivyoteka. Maana ya jina la Melkisedeki, kwanza ni “Mufalme wa haki,” tena ni mufalme wa Salemu, ni kusema “Mufalme wa amani.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 7:2
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nalo jiwe hili nililosimika hapa kama nguzo, litakuwa nyumba yako Mungu, nami nitakupa sehemu ya kumi ya vitu vyote utakavyonipa.”


Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,


Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.


Hata hivyo, utapata mwana ambaye atatawala kwa amani kwa sababu nitamupa amani na waadui zake wote wa jirani. Jina lake litakuwa Solomono, kwa maana katika siku za utawala wake, atailetea inchi ya Israeli amani na utulivu.


Haki istawi maisha yake yote, na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.


Kuelekea mifugo, kila nyama wa kumi ni mutakatifu kwa Yawe.


Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.


Kuelekea Walawi, hao nimewapa sehemu ya kumi ya kila kitu Waisraeli wanachonitolea kuwa urizi wao. Haya yatakuwa malipo yao kwa kazi wanayotoa katika kulitunza hema la mukutano.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


“Sifa kwa Mungu juu mbinguni, na amani katika dunia kwa watu anaowapenda.”


Huyu Melkisedeki alikuwa mufalme wa Salemu na kuhani wa Mungu Mukubwa. Abrahamu alipokuwa akirudi toka katika vita nyuma ya kuwashinda wafalme wane, Melkisedeki alikutana naye na kumubariki,


Hakuna mambo yaliyoandikwa juu ya baba ya Melkisedeki, wala mama yake, wala majina ya babu zake. Tena, habari za kuzaliwa kwake na za kufa kwake hazijulikani. Anafanana na Mwana wa Mungu kwa kuwa yeye ni kuhani kwa milele.


Atatwaa sehemu ya kumi ya ngano zenu na ya zabibu zenu na kuwapa wakubwa wake na watumishi wake.


Atatwaa sehemu ya kumi ya kondoo wenu. Na ninyi wenyewe mutakuwa watumwa wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ