Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 7:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 kwa maana Sheria ya Musa haikuleta ukamilifu. Lakini sasa kumeletwa tumaini nzuri zaidi, na kwa njia ya tumaini hili tunaweza kumukaribia Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 7:19
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini, kwangu ni vizuri kuwa karibu na Mungu. Wewe Bwana wangu Yawe ndiwe usalama wangu. Nitatangaza mambo yote uliyotenda!


Nilipokuita ulifika karibu nami ukaniambia: Usiogope!


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.


Tuseme nini basi? Sheria ni zambi? Hapana hata kidogo! Lakini pasipo Sheria singejua zambi ni nini. Kwa maana singejua kutamani ni nini kama Sheria isingesema: “Usitamani.”


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Lakini, tunajua kwamba mutu hahesabiwi haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, lakini kwa njia ya kuamini Yesu Kristo. Sisi vilevile tumeamini Yesu Kristo kusudi tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika yeye, wala si kwa njia ya kushika Sheria. Ni vile kwa maana hakuna mutu atakayehesabiwa haki kwa njia ya kushika Sheria.


Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.


Hivi Sheria ilikuwa kama mwangalizi wetu mpaka Kristo alipofika, kusudi tuhesabiwe haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani.


Na katika kuungana kwetu na Yesu Kristo na kwa njia ya kumwamini tunapata uhuru wa kufika mbele ya Mungu tukiwa na tumaini kubwa.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tunayemutumainia.


Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.


kwa maana Mungu alikuwa ametayarisha mambo mazuri zaidi kwa ajili yetu kusudi wao wenyewe wasipate kukamilishwa bila sisi vilevile.


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


Ukuhani ndio ulikuwa musingi wa Sheria iliyotolewa kwa Waisraeli. Basi ikiwa ukamilifu ulipatikana kwa njia ya kazi ya ukuhani wa uzao wa Lawi, hakungekuwa tena lazima kutokee kuhani mwingine anayekuwa sawa na Melkisedeki, kwa pahali pa kuhani anayekuwa sawa na Haruni.


Zaidi ya hii, mambo yale yalifanyika kufuatana na kiapo cha Mungu. Wale makuhani wengine wa uzao wa Lawi waliwekwa kwa kazi yao pasipo kiapo.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Lakini sasa Yesu amepewa kazi inayokuwa bora zaidi kuliko kazi ya wale makuhani, kwa maana yeye ni mupatanishi wa agano linalokuwa zuri zaidi. Sherti za agano lile zinasimamia juu ya ahadi ya Mungu inayokuwa bora zaidi.


Huo ni mufano wa wakati wa sasa unaoonyesha kwamba matoleo na sadaka zinazotolewa kwa Mungu haziwezi kumufanya yule anayeabudu kuwa na moyo mukamilifu.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ