Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Huyu mwingine hakuwekwa kuwa kuhani kwa amri ya kimutu kufuatana na ukoo wake, lakini kufuatana na uwezo wa uzima usiokuwa na mwisho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 7:16
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tunajua kwamba Sheria inaelekea maisha ya kiroho, lakini mimi ni mutu wa kimwili, kwa maana nimeuzishwa kama vile mutumwa wa zambi.


Na sisi vilevile tulipokuwa tungali kama watoto, tulikuwa watumwa wa vitu vyenye uwezo vilivyotawala dunia.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Alifuta barua ya madeni yetu na sherti zilizotushitaki. Aliyafuta kabisa kwa kuyapigilia juu ya musalaba.


Ninyi mumekufa pamoja na Kristo na kukombolewa toka katika uwezo wa roho mbaya zinazotawala dunia. Kwa nini munaishi tena kama watu wa dunia mukilazimishwa kushika kanuni kama hizi:


Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.


Tena jambo hili linaloonyesha wazi zaidi maneno haya: kumetokea kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki.


Maana Maandiko Matakatifu yanashuhudia: “Wewe ni kuhani kwa milele kwa mufano wa Melkisedeki.”


Lakini Yesu amewekwa kuwa kuhani kwa njia ya kiapo, wakati Mungu alipomwambia: “Bwana ameapa, naye hatageuka: ‘Wewe ni kuhani kwa milele.’ ”


Sheria ya Musa inawaweka watu wenye uzaifu kuwa Makuhani Wakubwa, lakini kufuatana na kiapo kilichokuja nyuma ya Sheria ile, Mwana anayekuwa mukamilifu kwa milele aliwekwa kuwa Kuhani Mukubwa.


Hakuna mambo yaliyoandikwa juu ya baba ya Melkisedeki, wala mama yake, wala majina ya babu zake. Tena, habari za kuzaliwa kwake na za kufa kwake hazijulikani. Anafanana na Mwana wa Mungu kwa kuwa yeye ni kuhani kwa milele.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ