Nawe utakumbuka mienendo yako na kupata haya wakati nitakapokupa wadada zako, mukubwa na mudogo, kama wabinti zako, ingawa si kwa sababu ya agano kati yangu na wewe.
Ukuhani ndio ulikuwa musingi wa Sheria iliyotolewa kwa Waisraeli. Basi ikiwa ukamilifu ulipatikana kwa njia ya kazi ya ukuhani wa uzao wa Lawi, hakungekuwa tena lazima kutokee kuhani mwingine anayekuwa sawa na Melkisedeki, kwa pahali pa kuhani anayekuwa sawa na Haruni.
Naye Bwana wetu ambaye maneno haya yanamwelekea, alikuwa mutu wa kabila lingine, wala hakuna hata mutu mumoja wa kabila lake aliyefanya kazi ya ukuhani kwenye mazabahu.
Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.