Akamwita mutoto yule Noa, akisema: “Mutoto huyu ndiye atakayetufariji kutokana na kazi yetu ngumu tunayofanya kwa mikono yetu katika inchi ambayo Yawe alilaani.”
Huyo ni kama kichaka katika jangwa, hataona mazuri yoyote. Ataishi pahali penye kukauka katika jangwa, kwenye udongo ulioharibiwa na chumvi, na usiokaliwa na watu.
Yawe hakuweza kuvumilia tena matendo yenu maovu na mambo ya kuchukiza muliyotenda; ndiyo maana inchi yenu imekuwa ukiwa, jangwa, laana na bila wakaaji, kama inavyokuwa mpaka leo.
“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!
Halafu Yesu akalaani muti ule, akisema: “Tangia sasa hata milele, mutu asipate tena tunda tokea juu yako.” Nao wanafunzi wake wakasikia maneno hayo aliyosema.
Kama munavyojua, nyuma ya pale alikataliwa wakati alipotaka kupokea baraka toka kwa baba yake. Yeye hakukuwa tena na namna ya kugeuza tendo lake ijapokuwa alitafuta baraka ile kwa machozi.