Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 6:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Maana watu wanapokwisha kuangaziwa na ukweli wa Mungu na kuonja zawadi ya mbinguni, na kuishi katika ushirika na Roho Mutakatifu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 6:4
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuhani ataangalia nguo ile kisha kufuliwa. Ikiwa ile alama haijabadilika rangi yake hata ingawa taka halikuenea, basi, nguo ile ni chafu. Nguo ile utaichoma kwa moto, ikuwe alama ile iko nyuma au mbele ya nguo ile.


Ikiwa taka lile litatokea tena kisha kutoa mawe hayo na kukwaruza lipu na kuipiga lipu upya,


naye akasema mashairi haya ya Yawe: Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Peori mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho.


Halafu anakwenda kutwaa pepo wengine saba wanaokuwa wabaya kumupita, nao wote wanakuja kuingia na kukaa mule. Na hali ya mwisho ya mutu yule inageuka mbaya kuliko hali yake ya kwanza. Na hivi ndivyo itakavyokuwa kwa watu wa kizazi hiki kibaya.”


“Ninyi ni kama chumvi kwa watu wote. Lakini kama chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini ipate tena kukolea? Haifai tena hata kidogo, inabakilia kutupwa na kukanyagwa na watu.


Kama mutu asipokaa ndani yangu, yeye ni kama tawi linalotupwa na kukauka. Matawi yanayokauka yanakusanywa na kutupwa katika moto nayo yanateketea.


Yoane akawajibu: “Hakuna mutu anayeweza kuwa na kitu isipokuwa amekipewa na Mungu.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: Musa hakuwapa ninyi mukate wa mbinguni, lakini ni Baba yangu anayewapa ninyi mukate wa kweli wa mbinguni.


Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.


Basi ikiwa Mungu aliwapa wale watu zawadi ile ile Roho Mutakatifu aliyotupatia sisi wakati tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nisubutu kupingana na Mungu?”


Naye Mungu anayejua mafikiri ya mutu, alihakikisha kwamba amewakubali watu wa mataifa mengine kwa njia ya kuwapatia Roho Mutakatifu sawa vile alivyotupatia sisi.


Lakini Petro akamujibu: “Feza yako ipotelee mbali pamoja nawe, kwa sababu umezani kwamba unaweza kununua ile zawadi ya Mungu kwa njia ya feza!


Kwa maana ninatamani sana kuonana nanyi, kusudi nigawanye pamoja nanyi zawadi ya kiroho, mupate kusimama imara.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Ninataka mujibu ulizo hili moja: mumepokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kushika Sheria au kwa sababu mumesikia na kuamini Habari Njema?


Mungu aliwajaza Roho wake na kufanya miujiza kati yenu kwa sababu munashika Sheria au kwa sababu munasikia na kuamini Habari Njema?


Ninaomba Mungu aifungue mioyo yenu ipate kuona mwangaza wake. Kwa hiyo mutapata kujua tumaini munalokuwa nalo kutokana na mwito wa Mungu. Vilevile mupate kujua utajiri mukubwa wa urizi anaouwekea watu wake,


Kwa maana mumeokolewa kwa neema ya Mungu, kwa njia ya imani. Jambo hili halitokani na ninyi wenyewe, lakini ni zawadi ya Mungu.


Nimewekwa kuwa mutumishi wa Habari Njema kwa njia ya zawadi Mungu aliyonipatia kutokana na uwezo wake.


Lakini kila mutu kati yetu alipokea neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.


Usiache kutumia ile zawadi ya kiroho inayokuwa ndani yako, uliyopokea kutokana na maneno ya manabii na kwa njia ya kuwekewa mikono na wazee wa kanisa.


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Alesanduro, yule mufua vyuma amenitendea mabaya mengi. Bwana atamulipa kufuatana na matendo yake.


Mukumbuke mambo yaliyowatokea katika siku zilizopita. Ninyi mulipokwisha kuangaziwa na Mungu, mulipita katika mateso mengi lakini mulivumilia.


Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.


Mutu akimwona ndugu yake anafanya zambi isiyoleta kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, Mungu atamupa mutu yule uzima. Jambo hili linaelekea wale wanaotenda zambi isiyoleta kifo. Maana kuna zambi inayoleta kifo lakini sisemi kama ataomba juu ya hiyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ