Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 6:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 6:18
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Harakisha! Kimbilia kule, nami sitafanya lolote mpaka utakapofika kule.” Hivyo muji ule ukaitwa Soari.


Yoabu alipopata habari, alikimbilia katika hema ya Mungu na kushikilia pembe za mazabahu kwa maana alikuwa amemwunga Adonia mukono ingawa mbele hakukuwa na Abusaloma.


Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.


Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.


Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.


Wakitaka ulinzi wangu, basi, wafanye amani nami. Wafanye amani nami!


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Maana Yawe anasema hivi: Towashi anayeshika siku zangu za Sabato, anayefanya mambo yanayonipendeza, na kuchunga agano langu,


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Enyi wafungwa wenye tumaini, murudi kwenye ukuta wa muji wenu. Sasa mimi ninawatangazia: nitawarudishia mema mara mbili.


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Wakati ule katika Yerusalema kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Simeoni. Mutu huyo alikuwa mwenye haki na mwenye kuogopa Mungu. Alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa taifa la Israeli. Roho Mutakatifu alikuwa pamoja naye;


Basi, Mungu anayewapa watu nguvu ya kuvumilia na kufarijika awape kuwa na nia moja mukifuata mufano wa Kristo Yesu.


Kristo alitolewa na Mungu kuwa sadaka ya usamehe wa zambi kwa njia ya damu yake kwa ajili ya wenye kumwamini. Mungu alifanya hivi kwa kuonyesha haki yake. Zamani, katika uvumilivu wake, aliacha kuazibu zambi za watu. Lakini kwa wakati wa sasa anaonyesha haki yake kusudi akuwe mwenye haki na kumuhesabia haki kila mutu anayemwamini Yesu.


Hapana hata kidogo! Sherti Mungu ajulikane kuwa mwenye ukweli, na kila mutu kuwa mwongo, kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ee Mungu, sherti ujulikane kuwa mwenye haki katika masemi yako. Nawe ushinde wakati unaposhitakiwa.”


Nalo tumaini hili si la udanganyifu, kwa sababu Mungu amemimia upendo wake ndani ya mioyo yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.


Maisha yenu katika kuungana kwenu na Kristo si yanawatia ninyi nguvu? Nao upendo wake si unawafariji ninyi? Si munaishi katika ushirika na Roho Mutakatifu? Si muko na moyo mwema na wa huruma?


Lakini, inawapasa ninyi kuendelea na musingi imara katika imani, musitikiswe na kupoteza lile tumaini mulilopata wakati muliposikia Habari Njema. Mimi Paulo nimewekwa kuwa mutumishi wa kuhubiri Habari Njema ile iliyokwisha kutangazwa kwa watu wote katika dunia.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Imani yenu na upendo wenu vinakuwa na musingi katika tumaini mulilowekewa mbinguni. Mulisikia juu ya tumaini lile mara ya kwanza wakati mulipohubiriwa ujumbe wa ukweli ni kusema Habari Njema.


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tunayemutumainia.


Upigane vita nzuri kwa kuchunga imani yako, upate kujitwalia uzima wa milele Mungu aliokuitia wakati ulipoitikia imani yako mbele ya washuhuda wengi.


Kama tunakosa kuwa waaminifu, yeye anabaki mwaminifu. Kwa maana hawezi kujikana yeye mwenyewe.


Na kwa njia hiyo watapata tumaini la uzima wa milele, ambalo Mungu asiyesema uongo alituahidi mbele ya mwanzo wa nyakati.


Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.


Basi nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia!”


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Naye Mungu, kwa sababu alitaka kuonyesha wazi kwa wale watakaopokea ahadi kwamba yeye hawezi kubadilisha shauri lake hata kidogo, akaihakikisha kwa kiapo.


kwa maana Sheria ya Musa haikuleta ukamilifu. Lakini sasa kumeletwa tumaini nzuri zaidi, na kwa njia ya tumaini hili tunaweza kumukaribia Mungu.


Lakini Yesu amewekwa kuwa kuhani kwa njia ya kiapo, wakati Mungu alipomwambia: “Bwana ameapa, naye hatageuka: ‘Wewe ni kuhani kwa milele.’ ”


Mutu yeyote akimwua mutu bila kukusudia anaweza kukimbilia katika muji mumoja na hivyo anaweza kuepuka yule mutu anayekuwa na ruhusa ya kulipiza kisasi cha damu.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


Yule anayemwamini Mwana wa Mungu yuko na ushuhuda huu ndani yake. Lakini yule asiyemwamini Mungu, amemufanya Mungu kuwa mwongo, maana hakuaminia ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.


Na Mungu ambaye ni utukufu wa Israeli hadanganyi, wala habadilishi wazo lake. Yeye si mwanadamu hata apate kubadilisha mawazo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ