Waebrania 6:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Naye Mungu, kwa sababu alitaka kuonyesha wazi kwa wale watakaopokea ahadi kwamba yeye hawezi kubadilisha shauri lake hata kidogo, akaihakikisha kwa kiapo.
Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile.
Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.
Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.
Kwa maana watu wanapofanya kiapo, wanaapa kwa jina la mutu anayekuwa mukubwa kuliko wao wenyewe, nao uhakikisho wa kiapo kile unakomesha mabishano yote kati yao.
Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.
Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.
Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.
Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,
Vilevile, ninyi waume, mukae na wake wenu mukifahamu kwamba wao ni kiumbe kizaifu. Munapaswa vilevile kuwapa heshima kwa sababu watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima. Mufanye hivi kusudi maombi yenu yasizuizwe.