Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa maana sisi vilevile tumehubiriwa Habari Njema kama vile watu wale. Walisikia habari lakini haikuwafalia kitu, kwa maana wale walioisikia hawakuipokea kwa imani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 4:2
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Paulo na Barnaba wakawaambia bila woga: “Ilitupasa kwanza kuhubiri Neno la Mungu kwenu. Lakini kwa kuona mumelikataa na kujihesabu ninyi wenyewe kwamba uzima wa milele haufai kwenu, basi tunashugulika na watu wa mataifa mengine.


Hivi Mungu alimutuma mutumishi wake kwa ajili yenu kwanza, kusudi awabariki ninyi, akimugeuza kila mumoja wenu toka katika njia zake mbaya.”


Kutahiriwa kuna mafaa kama ukitii Sheria. Lakini usipotii Sheria, wewe unahesabiwa kama mutu asiyetahiriwa.


Tuseme nini basi? Ikiwa wamoja kati yao hawakukuwa waaminifu, jambo hilo litaweza kuonyesha kwamba Mungu ataacha kuwa mwaminifu?


Ninaweza vilevile kugawanya mali yangu yote kwa kulisha wamasikini na hata kutoa mwili wangu uunguzwe, lakini kama sina upendo, hakuna faida ninayopata.


Ninataka mujibu ulizo hili moja: mumepokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kushika Sheria au kwa sababu mumesikia na kuamini Habari Njema?


Vilevile Maandiko Matakatifu yalisema tangu zamani kwamba watu wa mataifa mengine watahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani yao. Kwa sababu Mungu alipasha kwanza Habari Njema hii kwa Abrahamu: “Kwa njia yako mataifa yote yatabarikiwa.”


Munakumbuka kwamba niliwahubiri Habari Njema kwa mara ya kwanza kwa sababu ya ugonjwa nilioupata.


Lakini ingawa nilisema hayo yote, ninyi hamukumwamini Yawe, Mungu wenu,


Kwa maana tulipohubiri Habari Njema kwenu, hatukuihubiri kwa maneno tu, lakini kwa uwezo na kwa musaada wa Roho Mutakatifu na kwa uhakika kabisa. Munajua namna gani tulivyoishi katikati yenu, kusudi tupate kuwafalia.


Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.


Wale waliokuwa wa kwanza kuhubiriwa Habari Njema hawakuingia kwenye mapumziko yale kwa sababu ya kutokuamini kwao. Ingawa vile ingali inawezekana kwa wengine kuingia.


Kwa sababu hiyo, mutupilie mbali mambo yote machafu na matendo ya uovu yanayozidi. Mupokee kwa unyenyekevu neno lile lililopandwa ndani yenu na linaloweza kuwaokoa.


Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ