Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 4:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 4:15
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Usimutese mugeni. Ninyi munajua hali ya kuwa mugeni, maana mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.


Walimuzika pamoja na waovu; katika kifo aliwekwa pamoja na watajiri, ingawa hakutesa watu hata kidogo, wala hakusema neno lolote la udanganyifu.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Hatavunja tete linalokunja, wala hatazimisha taa inayofifia, mpaka aiwezeshe haki kutawala.


Kisha Roho Mutakatifu akamwongoza Yesu kwenda katika jangwa kusudi ajaribiwe na Shetani.


“Ninyi ndio muliokuwa pamoja nami katika majaribu yangu.


Kule akajaribiwa na Shetani kwa muda wa siku makumi ine. Kwa muda ule, yeye hakukula kitu. Na wakati siku zile zilipotimia, akasikia njaa.


Nani kati yenu anaweza kuhakikisha kwamba nimefanya zambi? Ikiwa ninasema ukweli, kwa sababu gani hamuniamini?


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Basi, kwa kuwa tuko na Kuhani Mukubwa zaidi aliyeingia mbinguni, ndiye Yesu Mwana wa Mungu, tushikamane sana na imani tunayotangaza.


Kwa kuwa yeye mwenyewe ni muzaifu, anaweza kuwavumilia wale waliopotoka bila kujua.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Yeye hakutenda zambi, wala neno la udanganyifu halikutoka ndani ya kinywa chake.


Ninyi munajua kwamba Yesu Kristo alikuja kusudi aondoe zambi, na hakuna zambi ndani yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ