Waebrania 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Kwa maana yule anayeingia kwenye mapumziko anayotayarisha, anapumzika kwa kuwa amemaliza kazi zake zote kama vile Mungu alivyopumzika alipomaliza kazi zake.
Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.
Tena nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikisema: “Andika maneno haya: ‘Heri tangu sasa kwa watu wanaokufa wakimwamini Bwana!’ ” Naye Roho anasema: “Ndiyo, ni kweli. Watapumzika toka katika masumbuko yao, kwa maana matendo yao yatafuatana nao.”
Kila mumoja wao akapewa kanzu nyeupe, wakaambiwa wapumzike kwa muda kidogo mpaka wakati hesabu ya watumishi wenzao na wandugu watakaouawa vilevile kama wao itakapotimia.