Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 musifanye mioyo yenu kuwa migumu kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu, sawa siku ile walipomupima katika jangwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 3:8
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao hawakutii; walikuwa wagumu kama babu zao ambao hawakumwamini Yawe, Mungu wao.


Sasa musikuwe wenye mioyo migumu kama babu zenu lakini mumutii Yawe. Mukuje katika Pahali Patakatifu pake Yerusalema, ambako ametakasa milele, mumwabudu Yawe, Mungu wenu, kusudi asiwakasirikie.


Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.


Lakini wao na babu zetu wakakuwa na kiburi na wakakuwa wagumu wakakataa kufuata maagizo yako.


Yeye ni mwenye hekima sana na nguvu nyingi. Nani aliyepingana naye, akashinda?


Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa, wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.


Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.


Hata hivyo walimupima na kumwasi Mungu Mukubwa; wala hawakushika maagizo yake.


“Musikuwe wagumu kama kule Meriba, kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,


Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Lakini hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini wakazidi kufanya vichwa vyao kuwa vigumu na kuasi kuliko hata babu zenu.


Lakini alipoanza kuwa na kiburi, akakuwa na roho ngumu na mwenye majivuno, aliondolewa katika kiti chake cha kifalme, akanyanganywa utukufu wake.


Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka migumu, wameziba masikio yao, nao wamefunga macho yao, kusudi wasipate kuona, nao wasipate kusikia, wala wasipate kunigeukia, nami ningewaponyesha.’


Lakini wamoja wakakuwa na mioyo migumu hata wakakataa kuamini, wakaanza kusema vibaya juu ya Njia ya Bwana mbele ya mukutano. Kwa hiyo Paulo akajitenga nao, akaenda na wanafunzi peke yao. Na kila siku alibishana na watu katika chumba cha kufanyia usomi cha mutu mumoja aliyeitwa Tirano.


Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.


Kwa nini munafanya mioyo yenu kuwa migumu kama Wamisri na Mufalme wao? Mungu alipowachekelea Wamisri, hawakuwaacha Waisraeli waondoke, nao wakaondoka?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ