Daudi yeye mwenyewe, akiongozwa na Roho Mutakatifu, alisema: ‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu, mpaka nitakapoweka waadui zako chini ya miguu yako.’
“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.
Nao walipokuwa wakiondoka bila kupatana, Paulo akaongeza kuwaambia maneno haya tu: “Roho Mutakatifu alikuwa na sheria ya kusema hivi kwa babu zenu kwa njia ya nabii Isaya:
Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.
Maandiko Matakatifu yanasema: “Leo ikiwa munasikiliza sauti ya Mungu, musifanye mioyo yenu kuwa migumu kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu.”
Kwa sababu hii Mungu anaweka tena siku ingine inayoitwa “Leo”. Naye alisema juu ya siku ile nyuma ya miaka mingi kwa njia ya Daudi, kufuatana na Maandiko haya yaliyokwisha kutajwa mbele: “Leo kama munasikiliza sauti ya Mungu musifanye mioyo yenu kuwa migumu.”
Hivi Roho Mutakatifu alikuwa akionyesha kwamba njia ya kuingia katika Pahali Patakatifu Sana ilikuwa bado kufunguliwa kwa wakati wote ile Hema ya kwanza ilipokuwa ingali ikisimikwa.
Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.