Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?
Lakini Yawe akamwambia Musa na Haruni: Kwa sababu ninyi hamukuniamini mimi, wala kuniheshimu mbele ya macho ya Waisraeli, basi kwa sababu hiyo hamutaingiza watu hawa katika ile inchi niliyowapa.
Na Yawe alipowatuma kutoka Kadesi-Barnea, akisema ‘Muende murizi inchi ambayo nimewapatia’, hamukufuata amri ya Yawe, Mungu wenu. Hamukuamini wala hamukutii yale aliyowaambia.
Kwa maana sisi vilevile tumehubiriwa Habari Njema kama vile watu wale. Walisikia habari lakini haikuwafalia kitu, kwa maana wale walioisikia hawakuipokea kwa imani.
Wale waliokuwa wa kwanza kuhubiriwa Habari Njema hawakuingia kwenye mapumziko yale kwa sababu ya kutokuamini kwao. Ingawa vile ingali inawezekana kwa wengine kuingia.