Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.
Imekuwa hivyo kwa sababu ya uovu walioufanya, wakanikasirikisha kwa kuifukizia ubani na kuitumikia miungu mingine ambayo wao wenyewe hawakuifahamu, wala ninyi, wala babu zenu.
Kwa nini munanichochea nikasirike kwa kuabudu sanamu mulizojitengenezea wenyewe na kuifukizia ubani miungu mingine katika inchi ya Misri ambamo mumekuja kuishi? Munataka kuangamizwa na kuwa laana na kuchekelewa mbele ya mataifa yote katika dunia?
Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?
Lakini kwa sababu mutumishi wangu Kalebu ni tofauti, na amenitii kwa ukamilifu, nitamufikisha kwenye inchi hiyo aliyoingia ndani yake na wazao wake watairizi.
Yawe alikuwa amesema kwamba wote watakufia katika jangwa, na kweli hakuna hata mumoja wao aliyebaki muzima, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.
Ijapokuwa mumekwisha kujua kabisa mambo haya yote, ninataka kuwakumbusha namna Bwana alivyowaokoa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, lakini kisha, akawaangamiza wale waliokataa kuamini.