Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waebrania 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waebrania 2:9
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajamwona Mwana wa Mutu akikuja katika Ufalme wake.”


“Kwa sababu gani munajisumbua kwa ajili ya nguo? Muangalie maua jinsi yanavyoota. Hayatumiki wala kujisukia nguo.


Na Yesu akaongeza kusema: “Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajaona Ufalme wa Mungu ukikuja kwa uwezo.”


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele ya kuona Ufalme wa Mungu unasimama.”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


“Baba ananipenda kwa sababu mimi mwenyewe ninajitoa kufa, kusudi nipate kuwa muzima tena.


Lakini mimi, nitakaponyanyuliwa toka katika dunia, nitawavuta watu wote kuja kwangu.”


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Basi kama vile kosa la mutu mumoja limewaletea watu wote azabu, ni hivi vilevile tendo la haki la mutu mumoja limewaweka huru na kuwapa uzima.


Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, kusudi wale wanaoishi, wasiishi kwa ajili yao wenyewe, lakini kwa ajili ya yule aliyekufa na kufufuka kwa ajili yao.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


aliyejitoa mwenyewe kusudi awakomboe watu wote. Na huo ni ushuhuda kwa wakati uliopangwa, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wake.


Unapenda haki na kuchukia uovu. Ni kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekusimika, akikupakaa mafuta, akikupatia heshima na kukuinua juu kuliko wenzako wote.”


Kwa sababu hii, wakati Kristo alipokuja katika dunia alisema: “Wewe haukutaka sadaka wala matoleo. Lakini umeniumbia mwili.


Kwa njia ya imani, Enoki alibebwa na Mungu toka katika dunia pasipo kufa. Naye hakuonekana tena, kwa sababu Mungu alimubeba mbinguni. Maana Maandiko Matakatifu yanasema kwamba mbele ya kubebwa kwake, Enoki alishuhudiwa kwamba alimupendeza Mungu.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Umemufanya kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika. Umemujaza utukufu na heshima.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Kila Kuhani Mukubwa anawekwa kusudi afanye kazi ya kutoa sadaka na matoleo. Kufuatana na hiyo, ilimupasa Kuhani wetu Mukubwa Kristo akuwe na kitu cha kutoa vilevile.


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


Macho yake yalimetameta kama ndimi za moto, na juu ya kichwa chake kulikuwa taji nyingi. Alikuwa na jina lililoandikwa juu yake, wala hakuna mutu aliyejua, isipokuwa yeye mwenyewe tu.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ